Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,

Gade chapit la Kopi




Yoshua 13:3
18 Referans Kwoze  

Na sasa itakufalia nini kwenda Misri kunywa maji ya muto Nili? Au itakufalia nini kwenda Asuria kunywa maji ya muto Furati?


Aliacha mataifa ya watu hawa: wakubwa watano wa Wafilistini, Wakanana wote, Wasidoni na Wahivi waliohamia katika milima ya Lebanoni kutoka mulima Bali-Hermoni mpaka kufikia Hamati.


Waavi walikuwa zamani wakiishi katika vijiji vya kando ya Mediteranea mpaka Gaza. Wakafutori kutoka kisiwa cha Kafutori wakawaangamiza, wakaishi humo pahali pao.)


Watu wakauliza: “Tutamutolea nini kwa malipo ya makosa?” Wao wakawajibu: “Sanamu tano za zahabu mufano wa majipu, na sanamu tano za zahabu mufano wa panya, kufuatana na hesabu ya wakubwa wa Wafilistini, maana kulikuwa pigo moja tu, kwa ninyi wote na kwa wakubwa wenu.


Hata hivyo, Wagesuri na Wamakati hawakufukuzwa lakini wanaishi kati ya Waisraeli mpaka leo.


Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misiraimu, Puti na Kanana.


Wakubwa wa Wafilistini wakamwendea Delila, wakamwambia: “Umubembeleze Samusoni kusudi ujue asili ya nguvu zake nyingi kusudi tuweze kumukamata na kumufunga. Ukifanya hivyo, kila mumoja wetu atakupa vikoroti makumi tatu vya feza.”


Nyuma ya Wafilistini kuliteka Sanduku la Mungu, walilibeba kutoka muji wa Ebeni-Ezeri mpaka katika muji wao wa Asidodi.


Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na Waisraeli wote. Nao walitoka tangu kwenye kiingilio cha Hamati, mpaka muto wa Misri.


walisafiri katika bahari nyingi. Mapato yenu yalikuwa ngano ya Misri, mukaweza kufanya biashara na mataifa.


Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Walituma wajumbe na kuwakusanya wakubwa wote wa Wafilistini na kuwauliza: “Tutafanya nini na Sanduku hili la Mungu wa Israeli?” Wakubwa wao wakajibu: “Sanduku hilo la Mungu wa Israeli mulipeleke Gati.” Basi, wakalipeleka kwenye muji wa Gati.


Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”


Kwa hiyo, Daudi akawakusanya Waisraeli wote katika inchi, tokea kwenye kijito cha Sihori kinachokuwa Misri, mpaka kwenye kiingilio cha Hamati kwa kulileta Sanduku la Agano toka Kiriati-Yearimu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite