Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 13:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Tena, Musa alikuwa ameipatia nusu ya kabila la Manase kulingana na ukoo zake,

Gade chapit la Kopi




Yoshua 13:29
10 Referans Kwoze  

Miji na vijiji hivi ndivyo watu wa kabila la Gadi walivyopewa kulingana na ukoo zao.


eneo la inchi kuanzia Mahanaimu mpaka kuingia katika inchi yote iliyokuwa ya mufalme Ogi katika Basani, pamoja na miji makumi sita ya Yairi,


Kisha eneo la kabila la Nafutali litafuata eneo la kabila la Manase, kutoka mashariki mpaka magaribi.


na kurizi inchi. Mukisha kufanya hayo, mutarudi, maana mutakuwa bila kosa mbele ya Yawe na wandugu zenu Waisraeli. Kisha Yawe atakubali inchi hii ya upande wa mashariki wa Yordani kuwa mali yenu.


Kwa hiyo, Musa akawapa watu wa ukoo wa Makiri mwana wa Manase, inchi ya Gileadi, nao wakakaa mule.


Kisha nikalipatia nusu ya lile kabila la Manase sehemu iliyobaki ya Gileadi pamoja na Basani yote iliyotawaliwa na Ogi, ni kusema eneo lote la Argobu. Inchi yote ya Basani ilijulikana kama vile inchi ya Warefai.


Kwa hiyo kabila la Manase liliongezewa sehemu mbili zaidi, ni kusema inchi ya Gileadi na Basani inayokuwa upande mwingine wa muto Yordani,


kwa sababu wabinti wa Manase waligawanyiwa sehemu zao kama vile wanaume wa kabila lao walivyogawanyiwa. (Wazao wengine wa Manase walipewa inchi ya Gileadi.)


“Murudie kwenu na utajiri mwingi; ngombe wenu wote, feza, zahabu, shaba, chuma na nguo nyingi. Mugawanyane na wandugu zenu vitu vyote mulivyonyanganya kutoka kwa waadui zenu.” Musa alikuwa amepatia nusu ya kabila la Manase sehemu yao kule Basani. Naye Yoshua akaipatia nusu ya pili ya kabila lile sehemu yao kule upande wa magaribi wa muto Yordani kama vile alivyoyapatia makabila yale mengine.


Nusu ya watu wa kabila la Manase waliishi katika inchi ya Basani. Hesabu yao iliongezeka kwa wingi sana, wakasambaa upande wa kaskazini mpaka Bali-Hermoni, Seniri na mulima Hermoni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite