Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 13:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 ilikuwa kuanzia Aroeri pembeni ya bonde la Arnoni na muji uliokuwa katika bonde hilo pamoja na inchi yote ya bonde ya Medeba.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 13:16
18 Referans Kwoze  

Eneo lao lilikuwa kuanzia Aroeri kandokando ya bonde la Arnoni na muji ule unaokuwa katikati ya bonde, na inchi ile yote ya bonde tangu Medeba mpaka Diboni,


Mufalme Sihoni wa Waamori aliyeishi kule Hesiboni na kutawala kutokea kwenye makao yake makubwa kule Aroeri, muji uliokuwa kandokando ya bonde la Arnoni. Alitawala vilevile kuanzia katikati ya bonde mpaka kwenye muto Yaboki ambao ulikuwa mupaka wa inchi ya Waamoni, ni kusema nusu ya inchi ya Gileadi.


Watu wa Hesiboni na Eleale wanalia, sauti zao zinasikilika mpaka Yasa. Hata waaskari wa Moabu wanalia kwa sauti; mioyo yao inatetemeka.


“Tulipoitwaa inchi hiyo, nikawapa makabila ya Rubeni na Gadi eneo la kuanzia upande wa kaskazini wa Aroeri karibu na Arnoni na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.


Sehemu ya inchi ambayo Musa aliwapa watu wa kabila la Rubeni kulingana na jamaa zao,


Ilikuwa vilevile pamoja na Hesiboni na miji yake yote inayokuwa katika sehemu ya bonde: ni kusema Diboni, Bamoti-Bali, Beti-Bali-Meoni,


wakaaji wa Aroeri, wakaaji wa Sifumoti, wakaaji wa Estemoa,


Walivuka muto Yordani wakianzia kuhesabu watu tangu Aroeri na muto unaokuwa katika bonde kuelekea Gadi mpaka Yazeri.


Walikopesha magari elfu makumi tatu na mawili, na mufalme wa Maka na waaskari wake akakuja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni walikusanyika toka kwenye miji yao yote, wakajiweka tayari kwa vita.


Hesiboni ulikuwa muji wa Sihoni mufalme wa Waamori, ambaye mbele alikuwa amepigana na mufalme wa Moabu na kuteka inchi yake yote mpaka muto Arnoni.


Musa alikuwa ameyapa yale makabila mawili na nusu sehemu yao upande wa mashariki wa Yordani, lakini Walawi hawakukuwa wamepewa sehemu yao pamoja nao.


Lakini Walawi hawatapata sehemu yoyote kati yenu, maana sehemu yao ni kuwa makuhani wa kumutumikia Yawe. Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase walikwisha kupata sehemu yao upande wa mashariki wa muto Yordani. Walipewa sehemu hii na Musa, mutumishi wa Yawe.”


Wakati wote Waisraeli walipoishi katika muji wa Hesiboni na vijiji vyake, na muji wa Aroeri na vijiji vyake pamoja na miji yote inayokuwa kwa ukingo wa muto Arnoni kwa muda wa miaka mia tatu, kwa nini haukulikomboa eneo hilo wakati huo?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite