Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mufalme Sihoni wa Waamori aliyeishi kule Hesiboni na kutawala kutokea kwenye makao yake makubwa kule Aroeri, muji uliokuwa kandokando ya bonde la Arnoni. Alitawala vilevile kuanzia katikati ya bonde mpaka kwenye muto Yaboki ambao ulikuwa mupaka wa inchi ya Waamoni, ni kusema nusu ya inchi ya Gileadi.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 12:2
12 Referans Kwoze  

Basi, akatanguliza zawadi zake, lakini yeye mwenyewe akalala katika kambi usiku ule.


kama vile Sihoni mufalme wa Waamori, Ogi mufalme wa Basani, na wafalme wote wa Kanana.


Ukawapatia ushindi juu ya falme na mataifa, ukawafanyia mengi kila upande. Wakashinda inchi ya Hesiboni iliyotawaliwa na mufalme Sihoni; na tena wakashinda inchi ya Basani iliyotawaliwa na mufalme Ogi.


Walilitwaa eneo lote la Waamori tangu muto Arnoni mpaka kwenye muto Yaboki na tangu katika jangwa upande wa mashariki mpaka kwenye muto Yordani upande wa magaribi.


Mufalme wa Amoni akawajibu hao wajumbe: “Waisraeli walipotoka Misri, walitwaa inchi yangu kutoka muto Arnoni mpaka kwenye muto Yaboki na muto Yordani. Sasa munirudishie inchi hiyo kwa amani.”


Bela mwana wa Ahazi na mujukuu wa Sema, wa ukoo wa Yoeli, uliokuwa ukiishi Aroeri na katika eneo lote la upande wa kaskazini mpaka Nebo na Bali-Meoni.


Enyi wakaaji wa Aroeri, musimame kandokando ya njia mupeleleze! Mumwulize yule anayekimbia na anayetoroka: Kumetokea nini?


Alifanya hivyo kisha Yawe kumushinda mufalme Sihoni wa Waamori ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Hesiboni, na mufalme Ogi wa Basani ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Astaroti na Edirei.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite