Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 11:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 11:8
13 Referans Kwoze  

vilevile eneo la milima inayokuwa kati ya Lebanoni na Misirepoti-Maimu ambayo wakaaji wake ni Wasidoni. Kadiri na jinsi Waisraeli watakavyoendelea mbele, mimi mwenyewe nitayafukuza mataifa hayo katika inchi hizo mbele yao. Nawe utawagawanyia Waisraeli sehemu mbalimbali za inchi hizo kwa kura kama nilivyokuamuru.


Eburoni, Rehobu, Hamoni, Kana mpaka Sidona muji mukubwa.


vilevile muji wa Hamati unaopakana na Hadiraki, na hata miji ya Tiro na Sidona ingawa inajiona kuwa na hekima sana.


Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.


Vilevile, akapeleka ujumbe kwa Wakanana waliokuwa pande za mashariki na magaribi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wayebusi ambao walikaa katika milima na kwa Wahivi ambao walikaa chini ya mulima Hermoni katika inchi ya Misipa.


“Zebuluni ataishi pembeni ya bahari, kivuko chake kitakuwa pahali pa kuegesha mashua. Mupaka wa inchi yake ni Sidona.


Kanana alikuwa babu ya Sidona, muzaliwa wake wa kwanza, na Heti,


Basi, kwa rafla kwenye chemichemi ya Meromu, Yoshua pamoja na waaskari wake wote akawatokea na kuwashambulia.


Umefezeheka, ewe Sidona, muji wenye upango kandokando ya bahari! Bahari yenyewe inatangaza: Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa, wala sijazaa; sikulea vijana wanaume, wala kukomalisha wabinti!


Vilevile, kisha Yawe, Mungu wenu, kuyatia katika mikono yenu, mutayashinda na kuyaangamiza kabisa. Musifanye agano lolote nayo wala musiyahurumie.


Mujue leo hii kwamba anayewatangulia kama vile moto unaoteketeza miti ni Yawe, Mungu wenu. Atawaangamiza na kuwashinda mbele yenu, kwa hiyo mutawafukuza na kuwaangamiza mara moja, kama vile Yawe alivyowaahidi.


Yoshua pamoja na Waisraeli wakawapiga na kuwaangamiza wote, na wachache wao walioponyoka wakakimbilia kwenye miji yao yenye kuta.


Kisha, wakaenda Gileadi halafu Kadesi katika inchi ya Wahiti, halafu wakafika Dani na kutoka Dani wakazunguka kwenda Sidona,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite