Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 11:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Waisraeli wakatwaa vitu vyote walivyonyanganya na nyama wa miji hiyo; lakini waliwaua wakaaji wake wote, wala hawakumwacha hata mutu mumoja.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 11:14
12 Referans Kwoze  

Kisha akauteketeza muji wa Hazori kwa moto na kuwaua wakaaji wake wote, hakumwacha hata mutu mumoja.


Basi, Yoshua aliiteka inchi yote; akawashinda wafalme wa sehemu za milima, eneo la Negebu, na sehemu za inchi ya bonde na miteremuko. Hakuacha kitu chochote chenye uzima lakini aliangamiza kila kitu kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.


Waisraeli waliteka tu nyama na mali kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua.


Lakini wanawake na watoto, ngombe, na vyote vinavyokuwa katika muji, vitu vyake vyote munaweza kuvibeba kwa ajili yenu wenyewe. Munaweza kufurahia vitu vya waadui zenu, ambavyo Yawe, Mungu wenu, amewapa.


Waisraeli wakawapeleka kuwa wafungwa wanawake wa Midiani na watoto wao. Wakanyanganya: ngombe, kondoo na mali yao yote.


Lakini katika miji ya inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa, musiache kitu chochote.


Lakini Waisraeli hawakuiteketeza miji iliyokuwa kwenye vilima, isipokuwa tu muji wa Hazori ambao Yoshua aliuteketeza.


Musa mutumishi wa Yawe aliipewa amri hii, naye Musa akamwamuru Yoshua ambaye aliitimiza. Yoshua alitimiza kila jambo Yawe alilomwamuru Musa.


Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”


Yosafati na waaskari wake wakaenda kukamata vitu. Wakakuta ngombe wengi, mali, nguo na vitu vingine vya bei kali. Iliwachukua muda wa siku tatu kusomba vitu hivyo, na hata hivyo, hawakuvimaliza maana vilikuwa vingi sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite