Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Wagibeoni wakapeleka ujumbe kwa Yoshua kule katika kambi Gilgali, wakamwambia: “Tafazali, usitutupilie sisi watumishi wako. Ukuje mbio utusaidie na kutuokoa kwa maana wafalme wote wa Waamori kutoka inchi ya milima wamekuja kutushambulia.”

Gade chapit la Kopi




Yoshua 10:6
14 Referans Kwoze  

Basi, wakamwendea Yoshua katika kambi kule Gilgali, wakamwambia yeye na Waisraeli: “Sisi tumetoka katika inchi ya mbali. Tafazali tunaomba mufanye agano nasi.”


Waisraeli walipokuwa wamepiga kambi kule Gilgali wakafanya sikukuu ya Pasaka magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi katika mabonde ya Yeriko.


Katika siku zile, Maria akafunga safari, akaenda kwa haraka katika muji mumoja uliokuwa katika vilima vya Yudea.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Kama vile milima inavyozunguka Yerusalema, ndivyo Yawe anavyozunguka watu wake, tangu sasa na hata milele.


Akatandika punda na kumwambia mutumishi: “Sasa kaza mwendo, wala usipunguze mpaka nitakapokuambia.”


Wakapewa Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni (Arba alikuwa baba ya Anaki), katika milima ya Yuda, pamoja na mbuga zilizoizunguka.


Yoshua akafanya nao mapatano ya amani; akafanya agano kwamba atawaruhusu kuishi. Viongozi wa Waisraeli wakawaapia kutimiza mapatano hayo.


Hivyo nikatwaa wale viongozi wenye hekima, akili na ujuzi ambao muliwachagua kutoka katika makabila yenu, nikawaweka kuwa viongozi wenu. Nikawaweka wengine kuwa majemadari wa makundi ya watu elfu moja moja, ya watu mia moja moja, ya watu makumi tano tano na ya watu kumi kumi. Nikachagua vilevile wakubwa wengine wa kuchunga kila kabila.


Waamaleki wanakaa katika eneo la Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanakaa katika eneo la milima, na Wakanana wanakaa karibu na bahari ya Mediteranea na karibu na kingo za muto Yordani.


Kisha wafalme hao watano wa Waamori: mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni, mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi na mufalme wa Eguloni, wakaunganisha waaskari wao, wakaenda nao mpaka Gibeoni. Wakapiga kambi kuuzunguka muji huo, wakaushambulia.


Basi, Yoshua pamoja na jeshi lake lote na mashujaa wakaondoka Gilgali.


Nao wakamwambia Yoshua: “Sisi tuko watumishi wako.” Naye Yoshua akawauliza: “Ninyi ni nani, na munatoka wapi?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite