Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 10:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Jua likasimama kimya na mwezi ukasimama mpaka taifa la Israeli lilipolipiza kisasi waadui zake. Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Yaseri, jua lilisimama kimya katikati ya mbingu, likakatiza safari yake ya kwenda kutua kwa siku nzima.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 10:13
29 Referans Kwoze  

Jua na mwezi vilikaa kimya katika makao yao, vilipoona mwangaza wa mishale yako ikienda mbio, vilipouona mukuki wako ukimetameta.


Nitafanya kivuli kwenye daraja iliyojengwa na Ahazi, kirudi nyuma hatua kumi. Nacho kivuli kikarudi nyuma hatua kumi.


Hakujakuwa siku kama hiyo hata kidogo wala haijapata kuonekana tena, siku ambayo Yawe amemwitikia mwanadamu kwa namna hiyo; maana Yawe mwenyewe aliwapigania Waisraeli.


Hapo Samusoni akamwomba Yawe: “Bwana wangu Yawe, ninakuomba unikumbuke. Unitie nguvu, mara hii moja tu, ee Mungu, kusudi niwalipize kisasi mara moja hii tu Wafilistini ambao waliyaongoa macho yangu mawili.”


Basi, Mungu hatawapatia haki wale wachaguliwa wake wanaomulilia usiku na muchana? Au atakawia kuwasaidia?


Inchi inatetemeka mbele yao, mbingu zinatikisika. Jua na mwezi vinatiwa giza, nazo nyota zinaacha kuangaza.


Mumusifu enyi jua na mwezi, mumusifu enyi nyota zote zinazoangaza.


Si kwa musemo au kwa maneno; wala hakuna sauti inayosikilika;


Mifano ya tangazo hili ambalo lilitolewa kama sheria katika kila jimbo ilisambazwa kwa kila mutu katika kila jimbo, kusudi Wayuda wajitayarishe kulipiza kisasi siku hiyo itakapofika.


Daudi alisema watu wa Yuda wafundishwe maombolezo hayo, nayo yameandikwa katika kitabu cha Yaseri. Daudi aliimba:


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Viongozi walijitokeza kuongoza Israeli, watu walijitolea kwa mapenzi yao. Mumushukuru Yawe!


Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.


Uwalipize kisasi Wamidiani mambo waliyowatendea Waisraeli; kisha wewe utakufa.


Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.


Kisha malaika wa ine akapiga baragumu. Sehemu moja ya tatu ya jua ikaharibishwa pamoja na sehemu moja ya tatu ya mwezi na ya nyota. Sehemu zile tatu zikaingiwa na giza. Hivi hakukuwa mwangaza kwa muda wa sehemu moja ya tatu ya saa za muchana na sehemu moja ya tatu ya saa za usiku vilevile.


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa sita, kukakuwa tetemeko kubwa la dunia; jua ikageuka kuwa nyeusi kama nguo ya kilio na mwezi ukageuka kuwa mwekundu kama damu.


Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”


Jua litatiwa giza, mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Bwana, ile siku kubwa na ya utukufu.


Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.


Kwa sababu hiyo, imeandikwa katika kitabu cha vita za Yawe: “Muji wa Wahebu katika inchi ya Sufa, na mabonde ya Arnoni,


“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.


Hezekia akamujibu: “Ni vyepesi zaidi kivuli kwenda mbele hatua kumi! Basi kirudi nyuma hatua kumi.”


Anaamuru jua lisipande, anafunika nyota zisiangaze.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite