Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 10:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 10:11
17 Referans Kwoze  

Bwana amejichagulia mutu wake shujaa na mwenye nguvu, ambaye ni kama mvua ya mawe na zoruba kali, kama zoruba ya mafuriko makubwa; kwa mukono wake atawatupa chini.


Nyota kutoka mbinguni zilishiriki vita, zilifuata njia zao zikapigana na Sisera.


Kisha mvua ya mawe makubwa yenye uzito wa zaidi ya kilo makumi ine ikanyesha juu ya watu. Nao wakamutukana Mungu kwa sababu ya hilo pigo la mvua ya mawe, kwa maana pigo lile lilileta hasara kubwa sana.


Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.


Sasa uwaambie hao manabii wanaopakaa chokaa ukuta huo kwamba kutanyesha mvua kubwa ya mawe na zoruba itavuma na ukuta huo utaanguka.


Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.


Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti; upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.


Halafu Yawe akateremusha moto mukali wa kiberiti kutoka mbinguni juu ya Sodoma na Gomora,


Umekwisha kuingia katika akiba za teluji, au kuona akiba za mvua ya mawe


maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayekwenda pamoja nanyi kupigana kwa ajili yenu mbele ya waadui zenu na kuwapa ushindi’.


Mapigano hayo yalienea katika inchi yote na watu wengi walikufa katika pori kuliko wale waliouawa kwa upanga katika vita.


ambavyo nimeviweka kwa ajili ya wakati wa fujo, kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?


Anaangusha mvua ya mawe kama makokoto, hakuna anayeweza kuvumilia baridi anayoituma.


Maana Yawe atasimama kama kule kwenye mulima Perasimu; atawaka hasira kama kule katika bonde la Gebeoni. Atatimiza mupango wake wa ajabu; atatenda kazi yake ya ajabu sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite