Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Ukuwe imara na hodari kwa sababu wewe utawaongoza watu hawa kuirizi inchi ambayo niliwaahidi kwamba nitawapa wazee wao.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 1:6
36 Referans Kwoze  

Akaniambia: Usiogope wewe unayependwa sana, uko salama. Ukuwe imara na hodari. Aliposema nami, nilipata nguvu, nikamwambia: Bwana, umekwisha kuniimarisha; sema kile ulichotaka kusema.


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Ukuwe tu imara na hodari. Ukuwe mwangalifu na kushika sheria yote mutumishi wangu Musa aliyokuamuru. Fuata kila sehemu ya sheria hiyo nawe utafanikiwa popote utakapoenda.


Basi kwa kumaliza, musimame imara katika kuungana kwenu na Bwana kwa uwezo wa nguvu zake kubwa.


Mukeshe, musimame imara katika imani, mukuwe hodari na wenye nguvu.


Basi wewe mwana wangu, ukuwe hodari kwa njia ya neema uliyopata katika kuungana kwako na Kristo Yesu.


Basi fanya angalisho na kukumbuka kwamba Yawe amekuchagua wewe umujengee nyumba ya ibada. Ukuwe hodari na utende hivyo.”


Ukiwa mwangalifu, na ukitii masharti na maagizo ambayo Yawe alimwagiza Musa juu ya Israeli, utastawi. Ujipe moyo, ukuwe imara. Usiogope wala usifazaike.


Hata hivyo, ujipe moyo, ewe Zerubabeli. –Ni ujumbe wa Yawe. Ujipe moyo, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki. Mujipe moyo nanyi watu wote wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe! Mufanye kazi, maana mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Umutegemee Yawe! Ujitie moyo, ukuwe hodari! Umutegemee Yawe!


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mujipe moyo! Sasa munayasikia maneno ambayo mulitangaziwa na manabii wakati musingi wa hekalu langu ulipowekwa kulijenga upya.


“Mwana wangu, kama inavyokuwa kawaida kwa viumbe vyote kufa, siku zangu zimekwisha. Ukuwe imara na hodari.


Ukae katika inchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyomupa baba yako Abrahamu, maana nitakupa wewe na wazao wako inchi hizi zote.


Sasa, enyi Wafilistini, mujipe moyo. Mukuwe hodari kusudi musipate kuwa watumwa wa Waebrania kama wao walivyokuwa watumwa wetu. Mukuwe hodari kama wanaume na kupigana.”


Kisha Yawe akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia: “Ukuwe imara na hodari, maana utawaongoza Waisraeli katika inchi ambayo nimewaapia kuwapa, nami nitakuwa pamoja nawe.”


Muangalie, Yawe, Mungu wenu, ameiweka inchi hii mbele yenu. Basi! Muende, muirizi kama vile Yawe, Mungu wa wazee wenu alivyowaambia. Musiogope wala musifazaike!’


“Mutii amri zote ninazowaamuru siku hii ya leo, kusudi mupate kuingia na kurizi inchi munayoiendea,


Lakini ujipe moyo! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu. Naye Yawe atutendee lile analoona ni jema kwake.”


Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Makabila haya yatagawanyiwa inchi ikuwe urizi wao, kulingana na hesabu ya majina yao.


Mutatwaa inchi hiyo na kukaa mule kwa sababu nimewapa muirizi.


Inchi hii yote nimeiweka mbele yenu. Basi, muende kutwaa inchi hiyo ambayo mimi Yawe niliapa kuwapa wazee wenu Abrahamu, Isaka, Yakobo na wazao wao.’ ”


Mutu yeyote atakayeasi amri yako au kukataa kutii maneno yako au jambo lolote unalomwamuru, atauawa. Lakini, wewe ukuwe na nguvu na kuwa hodari.”


Waisraeli walisafiri kwa muda wa miaka makumi ine katika jangwa hata wanaume wote waliokuwa na umri wa kwenda kwa vita wakaangamia kwa kuwa hawakusikiliza mambo Yawe aliyosema. Yawe alikuwa amewaapia watu hao kwamba hawataiona inchi ile inayotiririka maziwa na asali ambayo yeye aliwaapia baba zao kwamba atawapa.


Yoshua akawaambia: “Musiogope, wala musikuwe na wasiwasi, mukuwe imara na hodari, maana hivi ndivyo Yawe atakavyowatendea waadui zenu ambao mutapigana nao. Kwa hiyo, mukuwe imara na hodari.”


vilevile eneo la milima inayokuwa kati ya Lebanoni na Misirepoti-Maimu ambayo wakaaji wake ni Wasidoni. Kadiri na jinsi Waisraeli watakavyoendelea mbele, mimi mwenyewe nitayafukuza mataifa hayo katika inchi hizo mbele yao. Nawe utawagawanyia Waisraeli sehemu mbalimbali za inchi hizo kwa kura kama nilivyokuamuru.


Kwa hiyo, Yoshua akawaambia Waisraeli: “Mutangojea mpaka wakati gani kwenda kuikamata inchi ile ambayo Yawe, Mungu wa babu zenu, amewapatia?


Basi, Yawe aliwapa Waisraeli inchi yote ambayo alikuwa amewaahidi wazee wao. Nao wakairizi na kuishi mule.


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Lakini ninyi mujipe moyo, wala musiregee kwa maana mutapata malipo kwa kazi munayofanya.”


Si wewe, ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa inchi hii wakati watu wako Waisraeli walipoingia katika inchi hii, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako, ikuwe yao milele?


angalia, jinsi wanavyotulipa. Wanakuja kutuondoa katika inchi yako uliyoturizisha ikuwe urizi wetu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite