Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 1:5
34 Referans Kwoze  

Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayekwenda pamoja nanyi kupigana kwa ajili yenu mbele ya waadui zenu na kuwapa ushindi’.


Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii, nitaanza kukutukuza mbele ya watu wote wa Israeli kusudi wajue kwamba, kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo vilevile nitakavyokuwa pamoja nawe.


Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”


Lakini katika mambo haya yote tunapata ushindi kabisa kwa njia ya yule aliyetupenda.


Kama vile tulivyomutii Musa katika mambo yote, ndivyo tutakavyokutii wewe; Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na Musa.


Atawatia wafalme wao katika mikono yenu. Mutawaua, nao watasahaulika. Hakuna mutu yeyote atakayeweza kuwazuia, mpaka mutakapowaangamiza.


Basi, Yawe alikuwa pamoja na Yoshua na sifa zake zikaenea katika inchi yote.


Kisha Yawe akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia: “Ukuwe imara na hodari, maana utawaongoza Waisraeli katika inchi ambayo nimewaapia kuwapa, nami nitakuwa pamoja nawe.”


Yawe, Mungu wenu, ni Mungu mwenye rehema, hatawaachilia wala kuwaangamiza, wala kusahau agano ambalo alifanya na wazee wenu kwa kiapo.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hata kidogo maana nimewatia katika mikono yako, wala hakuna hata mumoja atakayeweza kukushinda.”


Kila mara Yawe alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi yule, akawaokoa toka katika mikono ya waadui zao muda wote wa maisha ya mwamuzi yule. Ingawa hivyo, Yawe aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na masumbuko yao.


Yawe akamwambia: “Nitakuwa pamoja nawe; nawe utawaangamiza Wamidiani sawa vile wangekuwa mutu mumoja.”


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Kama Yawe alivyokuwa pamoja na bwana wangu mufalme, akuwe vilevile na Solomono, na akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti cha kifalme cha bwana wangu mufalme Daudi.”


Mimi nitakaa kati ya wazao wa Waisraeli, na sitawaacha hata kidogo watu wangu, Waisraeli.”


Yawe, Mungu wetu, akuwe nasi kama alivyokuwa na babu zetu. Tunaomba asituachilie, wala asitutupilie.


Na kama utashika yote nitakayokuamuru, kama utaishi kulingana na mapenzi yangu, kama utatenda mema mbele yangu kwa kushika masharti yangu na amri zangu, kama vile mutumishi wangu Daudi alivyofanya, mimi nitakuwa pamoja nawe siku zote. Na nitakupatia inchi ya Israeli na kuufanya utawala wako ukuwe imara kama nilivyomufanyia Daudi.


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.


Wewe usiwaogope watu hao. Niko pamoja nawe kwa kukulinda. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mushambulizi atawatendea sawa anavyopenda; hakuna atakeyesubutu kupingana naye. Atasimama katika inchi tukufu, na inchi hiyo yote itakuwa chini ya mamlaka yake.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.


“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.


Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite