Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoshua 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wakamujibu Yoshua: “Mambo yote uliyotuamuru tutayafanya, na popote utakapotutuma tutakwenda.

Gade chapit la Kopi




Yoshua 1:16
10 Referans Kwoze  

Uwakumbushe watu wajinyenyekeze mbele ya watawala na wakubwa. Wanapaswa kuwatii na kuwa tayari kwa kufanya kila tendo zuri.


Heri wewe Musa uende karibu, usikilize yote Yawe, Mungu wetu, atakayosema, kisha ukuje kutuambia mambo hayo yote atakayokuambia. Sisi tutayasikiliza na kuyatimiza’.


Kisha, watu wa Gadi na wa Rubeni wakamwambia Musa: Sisi watumishi wako tutafanya kama vile ulivyotuamuru.


Mutawasaidia mpaka Yawe atakapowapa wandugu zenu vilevile pahali pa kupumzika, kama vile alivyowapa ninyi, nao vilevile warizi inchi ambayo wanapewa na Yawe, Mungu wenu. Kisha mutarudi katika inchi ambayo ni mali yenu na kuirizi, inchi ambayo mulipewa na Musa, mutumishi wa Yawe, ngambo ya muto Yordani.”


Kama vile tulivyomutii Musa katika mambo yote, ndivyo tutakavyokutii wewe; Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na Musa.


Watu wa Gadi na wa Rubeni wakajibu: Bwana, sisi tutafanya kama vile Yawe alivyotuambia sisi watumishi wako.


Yoshua mwana wa Nuni akajaa roho ya hekima, kwa sababu Musa alikuwa amemuwekea mikono yake. Hivyo Waisraeli wakamutii Yoshua na kufuata amri ambazo Yawe alimupa Musa.


Amuka utende, sisi tutakuunga mukono. Kwa hiyo ujipe moyo ufanye hivyo.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite