Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yona 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Alipofika, Yona aliingia katika muji. Kisha kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: Kunabaki siku makumi ine tu na muji huu wa Ninawe utaangamizwa!

Gade chapit la Kopi




Yona 3:4
10 Referans Kwoze  

Kama nabii akisema kitu aseme ni kwa jina la Yawe, na kitu hicho hakifanyiki au hakiko kweli, jambo hilo Yawe hakulisema; nabii amelisema kwa kiburi, nanyi musitishwe na jambo hilo.


Mungu alipoona walivyofanya, na jinsi walivyouacha uovu wao, akabadilisha nia yake, akaacha kuwatenda kama alivyokuwa amekusudia.


Nitakuongezea miaka kumi na mitano ya kuishi. Nitakuokoa wewe pamoja na muji huu toka katika mikono ya mufalme wa Asuria. Nitaulinda muji huu kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi.”


Wakati ule, Hezekia aligonjwa sana karibu kufa. Halafu nabii Isaya, mwana wa Amozi akamwendea, akamwambia: “Yawe amesema hivi: ‘Panga mambo yako sawasawa katika nyumba yako kwa sababu utakufa, hautapona.’ ”


Kwa Siku ya hukumu, watu wa Ninawe watasimama nanyi watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu wao waligeuka toka zambi zao waliposikia mahubiri ya Yona. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Yona!


Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa kitambulisho kwa watu wa Ninawe, ni vile Mwana wa Mutu atakavyokuwa kitambulisho kwa watu wa kizazi hiki.


Kwa Siku ya hukumu, watu wa Ninawe watasimama nanyi watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu wao waligeuka toka zambi zao waliposikia mahubiri ya Yona! Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Yona!


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Kama ninyi mutabaki katika inchi hii, basi, nitawasimamisha, wala sitawaharibu; nitawaotesha wala sitawaongoa; kwa maana nitabadilisha nia kwa sababu ya hasara niliyowatendea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite