2 Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uwatangazie watu ujumbe ninaokupa.
Wewe utawaambia maneno yangu, wakisikia au wakikataa kusikia, maana hao ni watu waasi.
Sasa basi, wewe Yeremia ujiweke tayari. Simama! Uende kuwaambia mambo yote ninayokuamuru. Usiwaogope, kusudi mimi nisikufanye kuwa mwoga mbele yao.
Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uukaripie. Maana uovu wake umenifikia.
Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”
Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu.
Basi, Yona akaondoka, akaenda Ninawe kama vile Yawe alivyomwagiza. Muji wa Ninawe ulikuwa mukubwa sana. Upana wake ulikuwa mwendo wa siku tatu.
Wewe mwanadamu, nimekuweka kuwa mulinzi wa Waisraeli. Utakuwa ukisikiliza maneno ninayokuambia na kwenda kuwatolea maonyo yangu.
Neno la Yawe lilimufikia Yona mara ya pili kusema hivi:
Naye Musa akamwambia Haruni maneno yote aliyoambiwa na Yawe ayaseme na vitambulisho vyote alivyoagizwa atende.
na kuwaamuru wao na wazao wao washike sikukuu za Purimu kwa wakati wake uliopangwa, kama vile walivyokuwa wanazikumbuka sheria za kufunga wakati wa kuomboleza. Maagizo haya yalitolewa na Mordekayi, Muyuda, pamoja na malkia Esteri.
Lakini Yawe akaniambia: Usiseme kwamba ungali kijana. Utakwenda kwa watu ninaokutuma kwao, na maneno yote nitakayokuamuru, utayasema.