Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yona 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Basi, Yona akiwa ndani ya tumbo la samaki yule, akamwomba Yawe Mungu wake,

Gade chapit la Kopi




Yona 2:2
26 Referans Kwoze  

Wimbo wa safari za kidini. Katika taabu yangu nilimwita Yawe, naye akanijibu.


Mumugeukie Mungu mupate kufurahi; nanyi hamutafezeheka hata kidogo.


Wema wako kwangu ni mwingi sana! Umeniokoa kutoka katika kuzimu.


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


Sasa, Daudi alikuwa katika matatizo makubwa kwa sababu watu wake walikuwa na uchungu katika roho zao kwa kupoteza watoto wao. Kwa hiyo wakakuwa wakitaka kumupiga mawe. Lakini Daudi alijipa moyo kwa kumutegemea Yawe, Mungu wake.


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Hatari ya kifo ilinizunguka, vitisho vya kaburi vilinishika; nilisongwa na mahangaiko na huzuni.


“Enyi munaomwabudu Yawe, mumusifu! Mumutukuze, enyi wazao wote wa Yakobo! Mumwogope Mungu, enyi wazao wote wa Israeli!


Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Zaburi ya Daudi.


Yesu alikuwa katika uchungu mukubwa, akazidi kuomba kwa bidii. Jasho iliyomutoka ikakuwa kama matone ya damu yaliyokuwa yakitiririka mpaka chini.]


Kuzimu nako kumechangamuka, kusudi ya kukupokea wakati utakapokuja. Kunaiamusha mizimu ikuje kukusalimia na wote waliokuwa wakubwa wa dunia; kunawasimamisha kutoka kwenye viti vyao vya kifalme wote waliokuwa wafalme wa mataifa.


Ee Mungu, unastahili sifa huko Sayuni. Watu wanapaswa kukutimizia viapo vyao,


Usikie kilio changu, ee Mungu, usikilize maombi yangu.


Kweli wewe unanikinga na nguvu za kuzimu, haumwachi mutakatifu wako aone kaburi.


maana hautaniachilia kubaki katika kuzimu, hautakubali mutumishi wako mutakatifu apate kuoza.


Usinizanie kuwa mimi ni mwanamuke asiyefaa kitu. Kwa muda wote huu nimekuwa nikisema mahangaiko yangu na taabu yangu.”


Kutoka chini ndani ya shimo, nilikulilia ee Yawe.


Nitakuteremusha ndani ya shimo kusudi ujiunge na wale wanaokuwa huko, walioishi zamani katika dunia; utakaa kule katika matongo kwa milele. Hautakaliwa na watu milele na hautakuwa na nafasi katika inchi za wanaokuwa wazima.


Hayo yameupata kusudi muti wowote unaokuwa pahali penye maji usiweze kurefuka tena kwa kimo hicho wala kukifikisha kilele chake katika mawingu. Muti wowote unaokunyweshwa maji usiweze tena kufikia urefu huo. Kwa maana kila kitu mwisho wake ni kifo; hata na watu vilevile. Wote watashiriki hali ya wanaoshuka katika shimo kwa wafu.


Wakati alipokuwa katika taabu, akamwomba Yawe, Mungu wake rehema. Akajinyenyekeza sana mbele ya Mungu wa babu zake.


Kwa maana kila mutu anayeomba anapewa; anayetafuta anapata, anayepiga hodi anafunguliwa mulango.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite