Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yona 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Lakini Yawe akavumisha upepo mukali katika bahari, kukatokea zoruba kali. Mashua ikakuwa karibu kuvunjika kabisa.

Gade chapit la Kopi




Yona 1:4
13 Referans Kwoze  

Mungu ndiye aliyeifanya milima, na kuumba upepo; ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake; ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku, na kukanyaga vilele vya dunia. Yawe wa majeshi ndilo jina lake!


Analeta mawingu kutoka miisho ya dunia, anapiga umeme na kunyesha mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Naye Yawe akaleta upepo mukali toka upande wa magaribi, ukawainua wale nzige na kuwasukumia kwenye bahari Nyekundu. Hakuna hata nzige mumoja aliyebaki katika inchi nzima ya Misri.


Nyuma ya pale, Yawe akavumisha upepo kwa rafla, ukaleta kwale kutoka katika bahari na kuwafanya watue kando ya kambi, mwendo wa siku moja hivi kila upande kuzunguka kambi, wakalundikana chini karibu metre moja hivi kwenda juu.


Lakini wewe uliuvumisha upepo wako, nayo bahari ikawafunika. Walizama ndani ya maji kama risasi.


Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, naye Yawe akasukuma bahari nyuma kwa upepo mukali toka upande wa mashariki. Upepo ule ulivuma usiku kucha, ukagawanya bahari sehemu mbili na katikati kukatokea inchi kavu.


Basi, Musa akainua fimbo yake juu ya inchi ya Misri. Yawe akaleta upepo toka upande wa mashariki, ukavuma juu ya inchi muchana kutwa na usiku kucha. Kulipokucha, ule upepo ukaleta nzige.


Yawe anafanya chochote anachotaka, mbinguni, katika dunia, ndani ya bahari na shimo ndefu.


Anapotoa sauti yake maji yanajikusanya mbinguni, anafanya ukungu upande kutoka mipaka ya dunia. Anafanya umeme upige wakati wa mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Mumusifu, enyi moto, mvua ya mawe na teluji, upepo wenye zoruba unaotimiza amri yake!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite