6 Wanapokaribia, watu wanajaa hofu, nyuso zao zinawaivya.
Munyanganye feza, munyanganye zahabu! Mali yake haina mwisho! Kuna wingi wa kila kitu cha bei kali!
Watu watafazaika, watashikwa na hofu na maumivu, watakuwa na uchungu kama mama anapozaa. Wataangalia kwa mashaka, nyuso zao zitaungua kwa haya.
Mujiulize sasa na kufahamu: Mwanaume anaweza kuzaa mutoto? Mbona basi, ninamwona kila mwanaume anajikamata kwenye kiuno kama mwanamuke anayesikia maumivu ya kuzaa na nyuso zimebadilika?
Sasa sura zao ni nyeusi kuliko makaa, wanapita katika barabara bila kujulikana; ngozi yao imebanana na mifupa yao, imekauka, imekuwa kama kuni.
Mimi ninavunjika moyo, ninaomboleza na kufazaika, kwa sababu watu wangu wameumizwa sana.
Nimekunjamana kama mufuko wa ngozi katika moshi, hata hivyo sijasahau masharti yako.
Muji wa Ninawe ni maangamizi matupu na uharibifu! Watu wamekufa moyo, magoti yanagongana, nguvu zimewaishia, nyuso zimebadilika!