Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoeli 2:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Usiogope, ewe inchi, lakini ufurahi na kushangilia, maana Yawe ametenda mambo makubwa.

Gade chapit la Kopi




Yoeli 2:21
21 Referans Kwoze  

Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Mbuga na inchi kavu vitachangamuka, jangwa litafurahi na kuchanua maua.


Kwa hiyo basi, mutulie na kulitazama jambo hilo kubwa ambalo Yawe atatenda mbele yenu.


vile vile nimekusudia kuutendea wema Yerusalema na watu wa Yuda. Basi, musiogope.


Nitawaondoa hao waadui wanaotoka kaskazini, nitawafukuza mpaka katika jangwa; waaskari wa mbele nitawatupa katika bahari ya Chumvi na wale wa nyuma katika bahari ya Mediteranea. Watatoa uvundo na harufu mbaya, hao ambao wamefanya maovu makubwa.


Basi, ninyi mumutii Yawe na kumutumikia kwa uaminifu, kwa moyo wenu wote. Mukumbuke yale mambo makubwa aliyowatendea.


“Mufikiri sana juu ya matukio ya zamani, mambo yaliyotukia mbele ninyi hamujazaliwa, tangu siku ile Mungu alipomwumba mutu katika dunia. Muulize katika ulimwengu wote, toka pembe moja mpaka nyingine, kama jambo la ajabu la namna hii limepata kutokea au kusikilika!


Enyi mito, mupige vigelegele; enyi vilima, muimbe pamoja kwa shangwe.


Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Nitakufanya muke wangu milele; ukuwe wangu kwa sheria na haki, kwa wema na huruma.


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Mutatoka Babeli kwa furaha; mutaongozwa muende kwa amani. Milima na vilima mbele yenu vitapiga kelele na kuimba, na miti yote katika mashamba itawapigia mikono.


Nguvu na haki yako, ee Mungu, vinafika mpaka juu katika mbingu. Wewe umefanya mambo makubwa sana. Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe?


Mutapata chakula kingi na kutosheka; mutalisifu jina la Yawe, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite