Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoeli 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?

Gade chapit la Kopi




Yoeli 2:17
42 Referans Kwoze  

Kisha akanipeleka mpaka katika uwanja wa ndani wa nyumba ya Yawe. Huko kwenye mulango wa hekalu, kati ya baraza na mazabahu, kulikuwa wanaume yapata makumi mbili na watano, wakigeuzia mugongo wao upande wa hekalu, na nyuso zao zikielekea upande wa mashariki. Walikuwa wanaabudu jua wakielekea upande wa mashariki.


Kwa nini mataifa yanasema: “Mungu wenu yuko wapi?”


Kwa nini mataifa yatuambie: “Mungu wenu yuko wapi?” Utujalie tuone jinsi utakavyowalipiza mataifa kisasi kwa ajili ya mauaji ya watumishi wako.


Na hivi mutabeba lazima ya damu iliyomwangwa katika dunia pasipo kosa, tangia kuuawa kwa Abeli aliyekuwa mukamilifu mpaka kuuawa kwa Zakaria, mwana wa Barakia, muliyemwuia kwenye hekalu katikati ya Pahali Patakatifu na mazabahu.


Niliwaona nzige hao wakikula na kumaliza kila jani katika inchi. Halafu nikasema: Ee Bwana wetu Yawe, ninakusihi utuhurumie! Wazao wa Yakobo wataweza kuishi namna gani? Wao ni wadogo sana!


Sadaka za vyakula na za kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Yawe. Makuhani, watumishi wa Yawe, wanaomboleza.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Uwanja wa baraza ya nyumba ulikuwa na upana wa metre ine na nusu toka upande mumoja wa nyumba mpaka upande mwingine. Na kina chake mbele ya hiyo nyumba kilikuwa metre tisa.


Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.


Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.


Halafu nikasema: Ee Bwana wetu Yawe, ninakusihi uache kuazibu! Wazao wa Yakobo wataweza kuishi namna gani? Wao ni wadogo sana!


Lakini nilijizuiza kufanya hivyo kwa heshima ya jina langu kusudi lisizarauliwe kati ya watu wa mataifa wanaoishi nao, hao walioona nikijijulisha kwa Waisraeli wakati wa kuwatoa katika inchi ya Misri.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Ee Bwana, ukumbuke matusi ya mutumishi wako, jinsi ninavyovumilia mazarau ya mataifa.


Umebomoa kuta zote za muji wake; umezivunjavunja nafasi zake za kukimbilia.


Tunazarauliwa na mataifa jirani, jirani zetu wanatuchekelea na kutusimanga.


Ee Mungu, mpaka wakati gani adui atakuchekelea? Watakufuru jina lako milele?


Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu: “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?”


Solomono akamutolea Yawe sadaka za kuteketeza juu ya mazabahu aliyokuwa amemujengea Yawe mbele ya baraza la hekalu.


isipokuwa tu kwa sababu ya majivuno ya waadui zao, kusudi waadui zao wasifikiri kwamba wamepata kuwaangamiza, nami Yawe sikufanya kitu katika mambo haya!


Yeye alimutumainia Mungu na alisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu. Ikiwa Mungu anapendezwa naye sasa amwokoe!”


Kwa hiyo sasa enyi makuhani, mumwombe Mungu kusudi atuhurumie. Yawe wa majeshi anasema hivi: Ikiwa munamutolea matoleo ya aina hiyo, kweli atawakubali?


Na leo tumekuwa watumwa; tuko watumwa katika inchi uliyowapa babu zetu kwa kufurahia matunda yake na mazao yake mema.


Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.


Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima. Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?


kwa sababu hiyo mimi nitawaongoa kutoka katika inchi hii ambayo nimewapa. Vielvile na nyumba hii ambayo nimeitakasa kwa ajili ya jina langu nitaitupilia mbali nami, na kuifanya kitu cha kuchekelewa na kuzarauliwa kati ya mataifa yote.”


basi, nitawahamisha watu wangu, Waisraeli, kutoka inchi hii ambayo nimewapa; vilevile na nyumba hii ambayo niliyoitakasa kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali nami, na kuifanya kitu cha kuchekelewa na kuzarauliwa kati ya watu wa mataifa yote.


Nanyi mutakuwa kinyaa, mazarau na mushangao kati ya watu wote wa inchi ambako Yawe atawapeleka.


Wakati huohuo mutu mumoja akamuleta mwanamuke mumoja Mumidiani katika nyumba yake, Musa na Waisraeli wote pamoja wakiwa wanaomboleza kwenye mulango wa hema la mukutano.


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Basi, Wakanana pamoja na wakaaji wote wa inchi hii watakapopata habari hiyo watatuzunguka na kutufuta kabisa katika dunia. Sasa utafanya nini kwa kuonyesha ukubwa wa jina lako?”


Machozi ni chakula changu muchana na usiku; ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”


Nimepondekana kwa ajili ya matukano yao, wanaponiuliza kila siku: “Mungu wako, yupo wapi?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite