6 Jeshi la nzige limeishambulia inchi yetu; lina nguvu na ni kubwa ajabu; meno yake ni kama ya simba, na mataya yake ni kama ya simba dike.
Nitawarudishia miaka ile iliyokuliwa na nzige, kila kitu kilichokuliwa na tunutu, parare na panzi, hilo kundi kubwa nililowaletea!
Kuna watu ambao meno yao ni kama upanga, na mataya yao ni kama visu. Wako tayari kuwatafuna wamasikini wa inchi, na wakosefu wanaokuwa kati ya watu!
Hawatakaa katika inchi ya Yawe. Watu wa Efuraimu watarudi katika utumwa kule Misri. Watakula vyakula vichafu kule Asuria.
juu ya inchi ya watu wangu inayoota miiba na michongoma, juu ya nyumba zote zilizojaa watu wenye furaha, juu ya muji uliokuwa na shangwe.
Utaingia ndani ya inchi ya Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka kwenye shingo. Utaenea juu ya inchi yako yote, ee Emanueli!
Udongo wenye mboleo akaugeuza kuwa udongo usioweza kutoa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.