Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoeli 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Ole kwetu kwa ile siku ya Yawe, siku hiyo ya Yawe inakaribia; inakuja pamoja na maangamizi, kutoka kwa Mungu Mukubwa.

Gade chapit la Kopi




Yoeli 1:15
18 Referans Kwoze  

Kweli, siku hiyo ni kubwa, hakuna ingine kama hiyo; ni siku ya taabu kwa watu wa Yakobo; hata hivyo, wataokolewa toka humo.


Yawe anaamuru kundi lake kwa sauti; waaskari wake ni wengi sana, wanaomutii hawahesabiki. Siku ya Yawe kweli ni kubwa na ya kutisha sana! Nani atakayeweza kuivumilia?


Kwa maana siku kubwa ya kasirani yao imekuja. Ni nani atakayeweza kusimama imara?”


Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango!


Lakini Yawe anamuchekelea mwovu, kwa maana anajua mwisho wake ni karibu.


Lakini siku hiyo ni siku ya Bwana wetu Yawe wa majeshi. Ni siku ya kulipiza kisasi, siku ya kuwaazibu waadui zake. Upanga utawamaliza hao na kutosheka, utaikunywa damu yao na kushiba. Maana Bwana wetu Yawe wa majeshi yuko na sadaka huko kaskazini karibu na muto Furati.


Kwa maana, siku hiyo imekaribia; siku ile ya Yawe iko karibu. Hiyo itakuwa siku ya mawingu ya kutisha, siku ya maangamizi kwa mataifa.


Siku inakaribia ambapo mimi Yawe nitayahukumu mataifa yote. Kama vile mulivyowatendea wengine, ndivyo mutakavyotendewa, mutalipwa kulingana na matendo yenu.


Munyamaze mbele ya Bwana wenu Yawe, maana siku ya Yawe iko karibu. Yawe ametayarisha sadaka, naye amekwisha kutakasa waalikwa wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite