Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoeli 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Mashamba yamebaki matupu. Inchi inaomboleza, maana ngano imeharibiwa, divai imetoweka, mafuta yamekosekana.

Gade chapit la Kopi




Yoeli 1:10
19 Referans Kwoze  

Kwa hiyo, inchi yote inakauka, wakaaji wake wote wanaangamia pamoja na nyama na ndege; hata samaki wanaangamizwa.


Hawatapata chakula kutoka kiwanja cha kupepetea, hawatapata divai mupya kutoka kikamulio.


Wamelifanya kuwa tupu; nalo linalilia katika ukiwa wake. Inchi yote imekuwa jangwa, wala hakuna mutu anayejali.


Enyi walevi, muamuke na kulia; enyi walevi wa divai, mulalamike; zabibu zote za kutengeneza divai mupya zimeharibiwa.


Nimeleta ukavu katika inchi, juu ya vilima na mashamba ya ngano, mashamba ya mizabibu na mashamba ya mizeituni na kila mumea, watu na nyama, na chochote mulichokitoshea jasho. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Mizabibu imenyauka, mitini imekauka, miti yote ya matunda imekauka. Furaha imetoweka kati ya watu.


Furaha na shangwe zimeondolewa kutoka inchi ya Moabu yenye mboleo. Nimeikomesha divai kutoka katika vikamulio. Hakuna mutu anayekamua mizabibu kwa shangwe; kelele zinazosikilika si za shangwe.


Mpaka wakati gani inchi itaomboleza kwa kukauka, na nyasi za mashamba yote kunyauka? Nyama na ndege wanakufa kwa uovu wa wakaaji wake. Wao wanasema: Mungu hataona mwisho wetu.


Kuna kilio katika barabara kwa kukosa divai; shangwe yote imekoma, furaha imetoweka katika dunia.


Mutatumia nguvu zenu bure maana mashamba yenu hayatatoa mavuno na inchi yenu haitazaa matunda.


Unapolima udongo, hautakupatia tena mazao yake. Utakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia.”


Kijito cha Nimurimu kimekauka; nyasi zimekauka, majani mabichi yamenyauka, hakuna chochote kinachoota hapo.


Mizabibu inanyauka, divai inakosekana. Wote waliokuwa wenye furaha sasa wanaugua kwa huzuni.


Alisikiliza, akajibu maombi yao, akasema: Sasa nitawapa tena ngano, divai na mafuta, nanyi mutashiba navyo. Sitawafanya muzarauliwe tena na mataifa.


Hata kama miti ya tini isipochanua maua wala mizabibu kuzaa zabibu, hata kama mizeituni isipozaa zeituni na mashamba yasipotoa chakula, hata kama kondoo wakitoweka katika zizi na nyama wa kufugwa kukosekana katika mazizi,


Nitawaazibu watoto wenu na ninyi wenyewe kutokana na uovu wenu, na kuzipakaa nyuso zenu mavi ya nyama wenu wa sadaka. Nitawafukuza mbali nami.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite