Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yobu 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Alikuwa na mali, kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, ngombe elfu moja, punda dike mia tano, na watumishi wengi sana. Yeye alikuwa wa heshima kuliko watu wote kule upande wa mashariki.

Gade chapit la Kopi




Yobu 1:3
34 Referans Kwoze  

Niliwatangulia kwa kuwaongoza, nikawaonyesha njia. Nilikuwa kwao kama vile mufalme kati ya majeshi yake; kama vile mutu anayewafariji wenye musiba.


Katika miaka ya Yobu iliyofuata, Yawe alimubariki zaidi kuliko hata alivyokuwa amemubariki pale mbele. Basi Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine, ngamia elfu sita, ngombe elfu mbili na punda dike elfu moja.


Kila mara Waisraeli walipopanda mbegu katika mashamba, Wamidiani, Waamaleki na watu wengine wa kule upande wa mashariki walikuja kuwashambulia.


Balamu akamutolea Balaki mashairi yake, akasema: Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, hakika, mufalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki: Kuja uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, hakika, kuja uwakaripie Waisraeli!


Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.


Naye akamutendea Abramu mema kwa ajili ya Sarai. Akamupa kondoo, ngombe, punda dume, watumishi na wajakazi, punda dike na ngamia.


Alitwaa Sarai muke wake, na Loti mwana wa ndugu yake, pamoja na mali yao yote na watu wote waliokuwa wamejipatia kule Harani, wakaondoka kuelekea inchi ya Kanana. Walipoingia katika inchi ya Kanana,


Yakobo aliendelea na safari yake, akafika katika inchi za watu wa upande wa mashariki.


Hesabu ya nyama wao ilikuwa kubwa sana hata inchi ile haikuweza kutosha kwa Abramu na Loti kuishi pamoja.


Vile vile alijiongezea miji kwa ajili yake mwenyewe, makundi mengi ya ngombe na kondoo kwa sababu Yawe alimupa mali nyingi.


Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.


Mufalme Mesha wa Moabu alikuwa mufugaji wa kondoo, na kila mwaka alilipa kodi kwa mufalme wa Israeli wana-kondoo elfu mia moja na manyoya ya kondoo wengine elfu mia moja.


Kulikuwa mutu mumoja kule katika muji wa Maoni ambaye alikuwa na biashara ya kondoo katika muji wa Karmeli. Kule Karmeli alifuga kondoo wake na kuwakata manyoya. Alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja.


Waadui waliozoea kuja kwa wingi kama nzige, pamoja na ngombe na ngamia wao na kufanya makao yao katika inchi ya Israeli, waliharibu inchi ya Israeli kwa vile walikuwa wengi sana wasiohesabika.


Hamuoni kwamba nyama wao wa kufugwa na mali yao yote itakuwa mali yetu? Basi, tukubaliane nao kusudi wakae pamoja nasi.”


Lakini akawapa wana wa habara zake zawadi. Na wakati alipokuwa bado muzima, akawapeleka katika inchi ya upande wa mashariki, mbali na mwana wake Isaka.


Sadaka na Kivuli walikuwa kule Karkori pamoja na jeshi lao la watu elfu kumi na tano ambao ndio tu waliobaki kutoka jeshi la upande wa mashariki, maana wenzao elfu mia moja na makumi mbili waliuawa.


Wamidiani, Waamaleki na watu wote wa mashariki walilala katika bonde, wengi kama nzige, na ngamia wao wasiohesabika, wengi kama muchanga wa bahari.


Daudi aliipiga inchi hiyo pasipo kuacha mutu yeyote muzima, akuwe mwanaume au mwanamuke, akateka kondoo, ngombe, punda, ngamia na nguo; kisha akarudi na kufika kwa Akisi.


Mara kwa mara, wana wa Yobu walifanya karamu katika nyumba ya kila mumoja wakifuatana. Waliwaalika wadada zao kula na kunywa pamoja nao.


Si wewe mwenyewe unamulinda pande zote pamoja na jamaa yake na kila kitu anachokuwa nacho? Wewe umemubariki na mali yake imeongezeka katika inchi.


Ninyi munauliza: “Iko wapi nyumba ya yule mukubwa? Iko wapi nyumba mwovu alimoishi?”


sikupata kufurahia wingi wa utajiri wangu au kujivunia mapato mengi ya mikono yangu.


Ningemuhesabilia Mungu kila kitu nilichofanya, ningemwendea kama mwana wa mufalme.


Nyuma ya Yobu kuwaombea warafiki zake, Yawe akamurudishia Yobu hali yake ya kwanza. Akamupa mara mbili ya yote aliyokuwa nayo pale mbele.


Juu ya Kedari na falme za Hazori ambazo Nebukadneza mufalme wa Babeli alizishambulia na kuzishinda, Yawe anasema hivi: Simama uende kulishambulia kabila la Kedari! Uwaangamize watu wa mashariki!


Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!


Basi, Yakobo akalala pale usiku ule. Kisha akatenga sehemu ya mali yake, ikuwe zawadi kwa ndugu yake Esau:


Yule tajiri alikuwa na kondoo wengi na ngombe wengi.


Menahemu alipata feza hiyo kwa kuwalazimisha watajiri wa Israeli kutoa muchango wa vikoroti makumi tano vya feza kila mumoja. Halafu Puli hakukaa Israeli lakini akarudi katika inchi yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite