Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 9:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Yesu akawajibu: “Mungekuwa vipofu, hamungekuwa na zambi. Lakini kwa maana munajidai kwamba munaona, mungali katika zambi.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 9:41
9 Referans Kwoze  

Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Kwa maana tukifanya zambi kwa makusudi tukisha kutambua waziwazi ukweli, hakuna tena sadaka ingine inayoweza kutolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.


Unamwona mutu anayejiona kuwa mwenye hekima? Afazali kumutumainia mupumbafu kuliko yule.


wewe unasema: Mimi sina kosa; hakika hasira yake imegeuka mbali nami. Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema kwamba haukutenda zambi.


“Mutumishi anayejua mapenzi ya bwana wake, lakini anakosa kujiweka tayari na kutofanya sawa na mapenzi ya bwana yule, atapigwa fimbo nyingi.


Basi, mutu anayejua kutenda mema wala hayatendi, anafanya zambi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite