Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 9:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Musa, lakini hatujui pahali mutu yule anapotoka!”

Gade chapit la Kopi




Yoane 9:29
28 Referans Kwoze  

Yesu akawajibu: “Hata nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushuhuda wangu ni wa kweli, kwa sababu ninajua pahali nilipotoka na pahali ninapokwenda. Lakini ninyi hamujui pahali nilipotoka wala pahali ninapokwenda.


Lakini kwa ulinzi wa Mungu ningali muzima hata leo. Nami ninatoa ushuhuda kwa wadogo na wakubwa, wala sisemi maneno mengine yanayokuwa mbali na yale manabii na Musa waliyosema kwamba yatatokea.


Makutano walimusikiliza Paulo mpaka aliposema maneno yale. Kisha wakasema kwa nguvu: “Mumuteketeze mutu huyu! Mumwue, kwa maana hastahili kuishi!”


“Huyu Musa ndiye yule Waisraeli waliyemukataa, wakisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi?’ Mungu alimutuma kuwa mukubwa na mukombozi wao, akisaidiwa na yule malaika aliyemutokea katikati ya kichaka kinachowaka moto.


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


Wafarisayo wamoja wakasema: “Mutu huyu hakutoka kwa Mungu kwa sababu hashiki sheria ya siku ya Sabato.” Lakini wengine wakasema: “Mutu mwenye zambi anaweza kuonyesha kitambulisho kama hiki?” Basi kukatokea mikorogano kati yao.


Lakini tunajua pahali mutu huyu anapotoka. Kristo atakapokuja, hakuna mutu atakayejua pahali atakapotokea.”


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


na kusema: “Mutu huyu alisema kwamba anaweza kubomoa hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa muda wa siku tatu.”


Lakini wakati Wafarisayo waliposikia maneno yale, wakasema: “Ni Belzebuli, mukubwa wa pepo ndiye anayemupa mutu huyu uwezo wa kufukuza pepo.”


Kule katika kambi walimwonea Musa wivu, na Haruni, mutumishi mutakatifu wa Yawe.


Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.


Alimujulisha Musa njia zake, aliwaonyesha watu wa Israeli matendo yake makubwa.


Walikulilia wewe, wakaokolewa; walikutegemea, nao hawakufezeheka.


Yehu aliporudi kwa wenzake, mumoja wao alimwuliza: “Kuna shida yoyote? Mwenda-wazimu huyu alitaka nini kwako?” Yehu akawajibu: “Si munamujua yeye na namna yake ya kusema?”


Uwaambie wamutie katika gereza na kumukulisha mukate kidogo na maji, mpaka nitakaporudi salama.”


Hakujatokea tena nabii katika Israeli kama Musa, ambaye Yawe alisema naye uso kwa uso.


Hapo Musa akawaambia watu: Hivi ndivyo mutakavyotambua kwamba Yawe ndiye aliyenituma kufanya mambo haya yote, wala siyo kwa mapenzi yangu mwenyewe.


Basi Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu akasema hivi kwa sauti: “Ndiyo, ninyi munajidai kwamba munanijua na munajua pahali ninapotoka. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini aliyenituma ni mwenye ukweli. Ninyi hamumujui,


Naye akawajibu: “Kweli neno hili ni la kushangaza kusema kwamba hamujui pahali alipotoka, ijapokuwa ameniponyesha macho.


Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite