Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu alipokuwa akipita katika njia, akaona mutu mumoja aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa kwake.

Gade chapit la Kopi




Yoane 9:1
12 Referans Kwoze  

Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.


Wanafunzi wake wakamwuliza: “Mwalimu, kwa sababu gani mutu huyu alizaliwa kipofu? Ni kwa ajili ya malipizi ya zambi yake mwenyewe au zambi ya wazazi wake?”


Hapo vipofu wataona tena, na viziwi watasikia tena.


Yesu akaondoka toka pale, naye alipokuwa katika njia, vipofu wawili wakamufuata wakilalamika, wakisema: “Utuhurumie, Ee Mwana wa Daudi!”


Na kulikuwa vipofu wawili waliokuwa wakiikaa pembeni ya njia, nao wakasikia kwamba Yesu anapita. Kwa hiyo wakalalamika, wakisema: “Bwana, mwana wa Daudi, utusikilie huruma!”


Yesu akamwuliza baba ya mutoto: “Amekuwa na hali hii tangu wakati gani?” Baba yake akamujibu: “Ni tangu utoto wake.


Kati yao kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye ugonjwa wa kutokwa na damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Alikuwa ametumia mali yake yote kwa kulipa waganga, lakini hakuna hata mumoja wao ambaye aliweza kumuponyesha.


Pale kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa mugonjwa tangia miaka makumi tatu na minane.


Naye yule mutu aliyeponyeshwa kwa njia ya kitambulisho hiki, alikuwa na umri wa miaka zaidi ya makumi ine.


Kule akamwona mutu mumoja mwenye ugonjwa wa kupooza aliyeitwa Ainea aliyeshindwa kutoka ndani ya kitanda kwa muda wa miaka minane.


Kule Listra kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa kiwete tangia kuzaliwa. Yeye hakuweza kusimama wala kupima kutembea.


Wale wenyeji wa kule walipoona nyoka yule anajizingia kwa mukono wake wakasemezana: “Hakika mutu huyu ni mwuaji, kwa maana ijapokuwa alipona katika hatari ya bahari, kufuatana na azabu ya haki ya Mungu, kufa kwake kunatimia.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite