Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:55 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

55 Ninyi hamumujui, lakini mimi ninamujua. Kama ningesema kwamba simujui, ningekuwa mwongo kama ninyi. Lakini ninamujua na ninashika neno lake.

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:55
25 Referans Kwoze  

Basi wakamwuliza: “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu: “Hamunijui mimi wala hamumujui Baba yangu. Kama mungenijua mimi, mungemujua Baba yangu vilevile.”


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Kweli, kweli ninawaambia: kama mutu akishika maneno yangu, hatakufa hata milele.”


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Yule anayemwamini Mwana wa Mungu yuko na ushuhuda huu ndani yake. Lakini yule asiyemwamini Mungu, amemufanya Mungu kuwa mwongo, maana hakuaminia ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.


Lakini watawafanyia ninyi haya yote kwa ajili yangu, kwa sababu hawamujui yule aliyenituma.


Ni nani anayekuwa musema uongo? Ni yule anayekana kwamba Yesu si Kristo. Huyu ndiye mupinga Kristo, kwa maana anamukana Baba na Mwana.


Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Kwa maana nilipokuwa nikipitapita katika muji wenu nilichunguza nafasi zenu za kuabudia, nikaona hata mazabahu mamoja ambako waliyochora maandiko haya: ‘Kwa ajili ya mungu asiyejulikana.’ Basi yule munayemwabudu pasipo kumujua ndiye mimi ninayemuhubiri kwenu sasa.


Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma.


Watafanya hivi kwa sababu hawakumujua Baba wala mimi.


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


kama vile Baba anavyonijua mimi, na mimi ninavyomujua Baba. Vilevile mimi ninatoa maisha yangu kwa ajili ya kondoo wangu.


Yule aliyenituma ni pamoja nami; hakuniacha peke yangu, kwa sababu siku zote ninafanya maneno yanayomupendeza.”


Si kusema kwamba kuna mutu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; yeye ndiye aliyemwona Baba.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Matendo yao yanawazuia wasimurudilie Mungu wao. Wamejaa uzinzi ndani ya mioyo yao; hawanijui mimi Yawe.


Kila mutu ajiepushe na jirani yake, wala asimwaminie ndugu yake! Maana ndugu ni mudanganyifu na kila jirani ni musingiziaji.


Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.


Halafu Wayuda wakamwambia: “Sasa tunajua hakika kwamba uko na pepo! Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa vilevile, nawe unasema kwamba mutu akishika maneno yako, hatakufa hata milele.


Tukisema kwamba tunashirikiana naye, lakini tunaishi katika giza, tunasema uongo, nayo matendo yetu si ya kweli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite