Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:54 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

54 Yesu akajibu: “Kama nikijitafutia sifa yangu mwenyewe, sifa ile haina maana. Baba yangu ndiye anayenisifu, yule munayejidai kwamba ni Mungu wenu!

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:54
28 Referans Kwoze  

Mimi sijitafutii sifa yangu mwenyewe, lakini kuna mumoja anayeitafuta kwa ajili yangu, naye ndiye mwenye uwezo wa kuhukumu.


Si vizuri kula asali nyingi sana; vilevile haifai kujipendekeza sana.


Maana alipokea heshima na utukufu toka kwa Mungu Baba, wakati sauti yenye utukufu mukubwa toka kwa Mungu ilipomufikia ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana!”


Kwa maana, mutu anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, lakini ni yule anayesifiwa na Bwana.


Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akainua macho mbinguni na kusema: “Baba, wakati umetimia. Uonyeshe utukufu wa Mwana wako, kusudi Mwana wako aonyeshe utukufu wako vilevile.


Ninyi munafanya matendo yale baba yenu anayofanya.” Wakamujibu: “Sisi si watoto wa haramu. Tuko na baba mumoja, naye ndiye Mungu.”


Mutu anayesema kwa mamlaka yake mwenyewe, anajitafutia sifa yake mwenyewe. Lakini yeye anayetafuta sifa ya yule aliyemutuma, huyu ni mwenye ukweli wala hana ubaya wowote.


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.


Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia.


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


“Mimi sipokei sifa kutoka kwa watu.


Ni vile Yesu alivyofanya kitambulisho chake cha kwanza katika Kana ya Galilaya. Pale alionyesha utukufu wake na wanafunzi wake wakamwamini.


Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Si wangu”, maana ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite