Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:49 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

49 Yesu akajibu: “Mimi sina pepo, lakini ninamuheshimu Baba yangu, nanyi munanikosea heshima.

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:49
16 Referans Kwoze  

Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Mimi nimekutukuza wewe katika dunia kwa kuwa nimemaliza kazi ile uliyonipa.


Nami nitafanya chochote mutakachoomba kwa jina langu, kusudi Baba atukuzwe kwa njia ya Mwana.


Wakati Yesu aliposikia habari hii, akasema: “Tukio la ugonjwa huu si la kumwua, lakini shabaha yake ni kuonyesha utukufu wa Mungu na kusudi Mwana wa Mungu atukuzwe.”


Yule aliyenituma ni pamoja nami; hakuniacha peke yangu, kwa sababu siku zote ninafanya maneno yanayomupendeza.”


Aliniambia: Wewe ni mutumishi wangu; kwa njia yako, ee Israeli, watu watanitukuza.


Kwa ajili ya uaminifu wake, Yawe, alipenda kutukuza sheria yake na kuiheshimisha.


Baba, utukuze jina lako!” Halafu sauti ikasikilika toka mbinguni ikisema: “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”


Watu wale wakajibu: “Wewe uko na pepo. Nani anatafuta kukuua?”


Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.


Hali ya asili yenyewe inawaonyesha kuwa ni haya kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu,


na hali ya utukufu; nao unazikwa katika uzaifu, lakini unafufuka na nguvu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite