Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu munakataa kukubali mafundisho yangu.

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:37
22 Referans Kwoze  

Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


wala si wote wanaotoka katika uzao wa Abrahamu, ndio watoto wa kweli wa Abrahamu. Kwa kuwa Mungu alimwahidia Abrahamu: “Ni kwa njia ya Isaka utapata wazao watakaoitwa wako.”


Kisha mambo hayo, Yesu akatembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayuda walitaka kumwua.


Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.


“Wandugu zangu, ninyi wazao wa Abrahamu na ninyi watu wa mataifa mengine munaokuwa hapa kwa kumwabudu Mungu, habari hii ya wokovu imetumwa kwetu!


Kwa sababu gani hamuelewi maneno ninayowaambia? Ni kwa sababu hamutaki kusikia maneno yangu.


Basi tangia siku ile wakakusudia kumwua Yesu.


Musa hakuwapa ninyi Sheria? Ingawa hivyo hakuna mumoja wenu anayetii Sheria. Na sasa sababu gani munatafuta kuniua?”


Halafu Wayuda wakaokota tena mawe kwa kumutupia.


Wao walisema hivi kwa kumupima, kusudi wapate sababu ya kumushitaki. Lakini Yesu akainama na kuandika juu ya udongo kwa kidole chake.


Halafu watu wamoja wa Yerusalema wakasema: “Huyu si mutu yule wanayetafuta kumwua?


Basi namna gani mutaweza kuamini, ninyi munaopokea sifa kutoka wamoja kwa wengine, lakini hamutafuti sifa inayotoka kwake anayekuwa Mungu peke yake?


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka migumu, wameziba masikio yao, nao wamefunga macho yao, kusudi wasipate kuona, nao wasipate kusikia, wala wasipate kunigeukia, nami ningewaponyesha.’


Wakamujibu: “Sisi ni wa uzao wa Abrahamu, wala hatujakuwa watumwa wa mutu hata siku moja. Namna gani basi unaweza kutuambia kwamba tutapata uhuru?”


Musijifikiri kwamba munaweza kujidai tu kuwa Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!


Baba yenu Abrahamu alishangilia akitumainia kuona siku ya kuja kwangu; na wakati alipoiona, alifurahi.”


Nimewaandikia ninyi watoto, kwa sababu mumemujua Baba. Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangia mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana, kwa sababu muko na nguvu na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mumemushinda yule Mwovu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite