Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Yule aliyenituma ni pamoja nami; hakuniacha peke yangu, kwa sababu siku zote ninafanya maneno yanayomupendeza.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:29
25 Referans Kwoze  

Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Kutakuwa wakati, nao umetimia, ndio wakati mutakaposambazwa, kila mutu akijiendea ngambo yake mwenyewe, nanyi mutaniacha peke yangu. Lakini mimi si peke yangu kabisa, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


“Siwezi kufanya kitu kwa mafikiri yangu mwenyewe. Ninahukumu tu kama vile Mungu anavyoniambia na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu sitafuti kufanya mapenzi yangu, lakini mapenzi ya yule aliyenituma.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Lakini hata ningehukumu, hukumu yangu ingekuwa ya kweli, kwa sababu sihukumu peke yangu, lakini Baba aliyenituma ni pamoja nami.


Watoto wangu wapendwa, ninawaandikia maneno hayo kusudi musitende zambi. Lakini kama mutu akitenda zambi, tuko na yule anayetutetea mbele ya Baba. Naye muteteaji yule ndiye Yesu Kristo, mwenye haki.


Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.


lakini sherti dunia ijue kama ninamupenda Baba, nami ninafanya kama alivyoniagiza. “Musimame, tutoke hapa.


Mimi nimekutukuza wewe katika dunia kwa kuwa nimemaliza kazi ile uliyonipa.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Mimi Yawe nimekuita kutenda haki, nimekushika mukono na kukulinda. Kwa njia yako nitafanya ahadi na watu wote, wewe utakuwa mwangaza wa mataifa.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Kwa ajili ya uaminifu wake, Yawe, alipenda kutukuza sheria yake na kuiheshimisha.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Bwana akulinde. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.


Lakini Yesu akamujibu: “Ukubali kufanya hivi sasa. Kwa maana ni kwa njia hii tutatimiza mambo yote yanayokuwa ya haki mbele ya Mungu.” Basi Yoane akakubali.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite