Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Nina maneno mengi ya kusema juu yenu na ya kuwahukumu. Lakini yule aliyenituma ni wa kweli, nami ninajulisha dunia maneno yale niliyosikia kwake.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:26
17 Referans Kwoze  

Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.


Lakini sasa munatafuta kuniua ijapokuwa nimewaambia ukweli niliousikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya vile.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Basi Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu akasema hivi kwa sauti: “Ndiyo, ninyi munajidai kwamba munanijua na munajua pahali ninapotoka. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini aliyenituma ni mwenye ukweli. Ninyi hamumujui,


Kama vile Mungu anavyokuwa mwaminifu, hakika mambo tuliyowaambia hayakukuwa ya kusema “Ndiyo” na “Hapana” kwa mara moja.


“Ningali na maneno mengi ya kuwaambia, lakini sasa hamujakuwa na uwezo wa kuyafahamu.


Yesu akawajibu: “Mafundisho ninayotoa si yangu, lakini ni ya yule aliyenituma.


Kweli, kweli ninakuambia: tunasema maneno tunayojua na kushuhudia maneno tuliyoona, lakini ninyi hamutaki kupokea ushuhuda wetu.


Basi wakamwuliza: “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu: “Mimi ni yule niliyewaambia tangu mwanzo.


Hawakujua kama alisema juu ya Baba yake.


Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite