Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ninajiendea, nanyi mutanitafuta, lakini mutakufa katika zambi zenu. Na zaidi ya hii hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:21
21 Referans Kwoze  

Mutanitafuta, lakini hamutaniona, kwa maana hamuwezi kufika pahali nitakapokuwa.”


Ni kwa sababu hii niliwaambia ninyi kama mutakufa katika zambi zenu. Musipoamini kwamba ‘Mimi Ndimi’, hakika mutakufa katika zambi zenu.”


Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.


Zamani ninyi mulikuwa mumekufa kiroho kwa sababu ya makosa na zambi zenu.


Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.


(Alisema hivi kwa kuonyesha ni kifo gani atakachokufa.)


Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”


“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!


Kwa maana ninawaambia, tangia sasa hamutaniona tena mpaka mutakaposema: ‘Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana.’ ”


Hakutakuwa tena vifo vya watoto wachanga, wazee nao hawatakufa mbele ya wakati wao. Mutu wa miaka mia moja akikufa, amekufa akiwa kijana; na akikufa mbele ya miaka mia moja, ni kusema amelaaniwa.


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


Mwovu akikufa, tumaini lake nalo linatoweka. Tumaini la asiyemwogopa Mungu ni la bure.


Japo alijisikia amejaa nguvu ya ujana, lakini italala pamoja naye katika mavumbi.


Ninakuapia kwa jina la Yawe, Mungu wako, Mwenye Uzima, kwamba mufalme amekuwa akikutafuta katika dunia yote. Na mufalme yeyote akisema kwamba haujaonekana kule, Ahabu alimutaka huyo mufalme aape na watu wake kwamba kweli hauko.


Yeye anasema kwamba tutamutafuta, lakini hatutamwona, na kwamba hatuwezi kufika pahali atakapokwenda. Maana ya maneno haya ni gani?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite