Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mwanamuke yule akamujibu: “Bwana, hakuna mutu.” Basi Yesu akamwambia: “Mimi vilevile sikuhukumu. Ujiendee, lakini usifanye zambi tena.”]

Gade chapit la Kopi




Yoane 8:11
27 Referans Kwoze  

Mungu hakumutuma Mwana wake katika ulimwengu kusudi ahukumu ulimwengu, lakini kusudi ulimwengu uokolewe naye.


Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”


Ninyi munahukumu kwa kufuatana na mafikiri ya kimutu; lakini mimi simuhukumu mutu.


Vilevile ninawaambia, ndivyo kutakuwa furaha kubwa zaidi mbinguni kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake, kuliko wenye haki makumi tisa na tisa wasiokuwa na lazima ya kugeuka toka zambi zao.


Sikukuja kuwaita wenye haki, lakini wenye zambi kusudi wageuke toka zambi zao.”


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Labda mutu atamwambia Mungu hivi: “Nimekosa, sitatenda zambi tena.


Au haujali na uwingi wa wema, utulivu na uvumilivu wa Mungu? Haujui kwamba wema wake ungeweza kukuongoza hata upate kugeuka toka zambi?


Hakika si vile, lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.


Vilevile ninawaambia, ndivyo wamalaika wa Mungu wanavyofurahi kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake.”


Yesu akajibu: “Ufalme wangu si wa dunia hii. Ufalme wangu ungekuwa wa dunia hii, watumishi wangu wangenipigania kusudi nisitolewe kwa Wayuda. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa katika dunia.”


Kwa hivi ilitupasa kushangilia na kufurahi, kwa maana mudogo wako huyu alikuwa amekufa na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ ”


Hakika si vile: lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.”


Mumutafute Yawe wakati angali anaweza kupatikana, mumwombe musaada wakati angali karibu.


na huko mutawaendea makuhani wa Kilawi, na mwamuzi ambaye yuko katika kazi kwa wakati huo, nanyi mutatoa mashitaki kwao nao watawatangazia uamuzi wao.


“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.


Mutambue kwamba njia ya kuvumilia kwa Bwana wetu ni wakati muzuri anaowapatia kusudi mupate kuokolewa. Na hiyo ni kufuatana na vile ndugu yetu mupendwa Paulo alivyowaandikia akiongozwa na hekima aliyopewa na Mungu.


Basi si kazi yangu kuhukumu wale wanaokuwa wa inje ya kanisa. Mungu ndiye atakayewahukumu. Lakini ninyi hamupaswi kuhukumu watu wa kanisa lenu? Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mumwondoe mutu yule mubaya toka katikati yenu.”


Kisha wakaondoka kwenda katika kijiji kingine.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite