Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 7:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Siku ya mwisho ya sikukuu ile iliyokuwa siku kubwa, Yesu akasimama na kusema hivi kwa sauti: “Mutu akiwa na kiu, akuje kwangu akunywe.

Gade chapit la Kopi




Yoane 7:37
50 Referans Kwoze  

Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


Yesu akawaambia: “Mimi ni mukate wa uzima. Anayenikubali hatasikia njaa hata kidogo, na yule anayeniamini hatasikia kiu hata kidogo.


Mutachota maji kwa furaha kutoka visima vya wokovu.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.


Kama pongo anavyotamani maji ya kijito, ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!


Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea.


Ninakunyooshea mikono yangu. Ninakuhitaji wewe, kama inchi kavu inavyohitaji mvua.


Kisha yule malaika akanionyesha muto wa maji ya uzima wenye kungaa kama kioo, uliokuwa ukitiririka toka kwenye kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.


Vilevile sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mumoja kusudi tukuwe mwili mumoja na sisi wote tumekunyweshwa Roho mumoja.


Mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Siku ya nane mutakuwa na mukutano mutakatifu. Musifanye kazi siku hiyo.


Hamuwezi kuchangia kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo. Vilevile hamuwezi kuchangia meza ya Bwana na meza ya pepo.


Wote walikunywa kinywaji kimoja cha kiroho; kwa maana walikunywa maji yaliyotoka ndani ya lile jiwe lililosafiri pamoja nao, nalo jiwe lilikuwa Kristo.


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Kwa muda wa siku saba mutatoa sadaka Yawe anazopewa kwa moto. Siku ya nane mutakuwa na mukutano mutakatifu na kumutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa. Mukutano huo ni mutakatifu. Siku hiyo musifanye kazi.


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Vilevile, nyuma ya kula akatwaa kikombe na kusema: “Kikombe hiki ni agano jipya la Mungu, linalohakikishwa kwa njia ya damu yangu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka kila mara munapokikunywa.”


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.


lakini ninyi hamutaki kuja kwangu mupate uzima.


Yoane akajibu: “Mimi ni sauti inayotangaza katika jangwa: ‘Munyooshe njia ya Bwana,’ ” sawa vile nabii Isaya alivyosema.


Yawe wa majeshi atawalinda watu wake, nao watawaangamiza waadui zao. Watapiga kelele katika vita kama walevi, wataimwanga damu ya waadui zao. Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.


Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Sauti inasema: Tangaza! Nami nikauliza: Nitangaze nini? Naye: Tangaza: wanadamu wote ni kama majani; usitawi wao ni kama maua ya shamba.


Kila siku, tangu siku ya kwanza mpaka ya mwisho, Ezra aliwasomea watu kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakafanya sikukuu ile kwa muda wa siku saba. Na siku ya nane wakafanya mukutano mukubwa wa kufunga sikukuu, kama vile ilivyoagizwa.


Kisha kuvuna mashamba yenu mutafanya sikukuu kwa muda wa siku saba, tangu siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba. Siku ya kwanza itakuwa siku ya mapumziko na hata siku ya nane.


Basi Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu akasema hivi kwa sauti: “Ndiyo, ninyi munajidai kwamba munanijua na munajua pahali ninapotoka. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini aliyenituma ni mwenye ukweli. Ninyi hamumujui,


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


Karibu na milango ya kuingilia katika muji, pahali wanapoingilia watu inaita kwa sauti:


Yoane ndiye yule Mungu aliyemutaja kwa njia ya nabii Isaya akisema: “Sauti inatangaza katika jangwa: ‘Mutengeneze njia ya Bwana, munyooshe pahali atakapopita!’ ”


Amewatuma wajakazi wake katika muji waite watu kutoka kwenye vilele vya milima:


Musikilize! Hekima inaita! Akili inapiga kelele yake!


Hekima inapiga kelele katika barabara, inaita kwa sauti kubwa katika viwanja;


Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.


Kila pahali muto huu utakapopita, kutaishi aina zote za nyama na samaki. Muto huu utayafanya maji ya bahari ya Chumvi kuwa maji baridi. Kokote utakakopita utaleta uzima.


Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


Yule mwanamuke akamwambia: “Bwana, hauna chombo cha kutekea, na kisima ni kirefu sana. Basi umepata wapi maji ya uzima?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite