Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 7:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Basi wakatafuta kumufunga, lakini hakuna mutu aliyemukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijatimia.

Gade chapit la Kopi




Yoane 7:30
22 Referans Kwoze  

Wakajaribu tena kumufunga Yesu, lakini akawaponyoka.


Yesu alisema maneno haya wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, kwenye sanduku za kuwekea matoleo. Hakuna mutu aliyemufunga, kwa sababu wakati wake ulikuwa haujatimia.


Na Yesu akawaambia: “Wakati unaofaa kwangu haujatimia; lakini wakati wowote unafaa kwenu.


Wafarisayo wakasikia maneno hayo watu waliyosemasema juu ya Yesu. Basi wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakatuma walinzi wao kumufunga.


Nao wakubwa wa makuhani na Wafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mutu akijua pahali Yesu alipokuwa, alete habari kusudi wapate kumufunga.


Imetupasa kufanya kazi za yule aliyenituma wakati kungali muchana, kwa sababu usiku unakaribia, wakati mutu asipoweza kutumika.


Kwa ajili ya hii, wakaokota mawe kwa kumutupia. Lakini Yesu akajificha na kutoka ndani ya hekalu.


Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu munakataa kukubali mafundisho yangu.


Musa hakuwapa ninyi Sheria? Ingawa hivyo hakuna mumoja wenu anayetii Sheria. Na sasa sababu gani munatafuta kuniua?”


Ninyi muende kwa sikukuu. Mimi sijaenda bado kwa sikukuu hii, kwa sababu wakati unaofaa kwangu haujatimia.”


Siku zote nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu, ninyi hamukunikamata. Lakini hii ni saa yenu; saa ya utawala wa bwana wa giza.”


Saa ile ile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakatafuta kumukamata, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao.


Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walipopata habari hii, wakatafuta njia ya kumwua Yesu. Lakini walimwogopa, kwa sababu kundi lote la watu walishangaa na mafundisho yake.


Kwa hiyo wakatafuta kumukamata, lakini waliogopa makundi ya watu kwa sababu wao walisadiki kwamba yeye ni nabii.


Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo, tangu zamani nilitangaza mambo yatakayotukia. Kusudio langu litatimia; mimi nitatimiza nia yangu yote.


wakati ulipoinuka kutimiza hukumu, kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.


Halafu Wayuda wakaokota tena mawe kwa kumutupia.


Wafarisayo wakaondoka pale na kwenda kufanya shauri la kumwua Yesu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite