Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 7:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Angalia, anasema waziwazi wala hawamwambii neno! Labda wakubwa nao wametambua kweli kuwa huyu ndiye Kristo.

Gade chapit la Kopi




Yoane 7:26
21 Referans Kwoze  

Ni nani kati ya wakubwa wetu au kati ya Wafarisayo aliyemwamini?


Kwa ajili ya kufungwa kwangu, wandugu wengi wamemwamini Bwana na kuwa na bidii sana ya kutangaza Neno la Mungu pasipo woga.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Hata hivi wengi kati ya wakubwa wa Wayuda wakamwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Wafarisayo, hawakushuhudia kwamba wameamini. Waliogopa kwamba watatengwa wasiingie katika nyumba ya kuabudia.


Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliogopa wakubwa wa Wayuda. Wakubwa wale walikuwa wamekwisha kupatana kwamba mutu yeyote anayesadiki kuwa Yesu ndiye Kristo, atatengwa asiingie katika nyumba ya kuabudia.


Lakini Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria walikataa mupango wa Mungu juu yao, na kukataa kubatizwa na Yoane.)


Halafu wakatuma kwake wamoja kati ya wanafunzi wao pamoja na watu wengine wamoja waliojiunga na Herode kumwuliza maneno haya: “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mutu wa kweli na kwamba unafundisha kwa kweli njia Mungu anayoamuru. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu yeyote kwa sababu hauangalii cheo cha mutu.


Yeye hataregea wala kuchoka, mpaka atakapoimarisha sheria yangu katika dunia. Watu wa mbali wanangojea mafundisho yake.


Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


Basi Pilato akafanya mukutano wa wakubwa wa makuhani, nao wasimamizi wa watu pamoja na watu wao.


Kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Nikodemo, mukubwa wa Wayuda, aliyekuwa mumoja wa kundi la Wafarisayo.


“Mukuje mumwone mutu aliyeniambia maneno yote niliyotenda. Huyu si Kristo?”


Halafu watu wamoja wa Yerusalema wakasema: “Huyu si mutu yule wanayetafuta kumwua?


Watu wengi katika kundi lililokuwa pale wakamwamini, wakisema: “Kristo atakapokuja, ataonyesha vitambulisho zaidi kuliko mutu huyu?”


Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite