Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 7:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Wayuda wakashangaa, wakisema: “Mutu huyu amepata elimu kama hii namna gani, naye hakufundishwa?”

Gade chapit la Kopi




Yoane 7:15
18 Referans Kwoze  

Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”


na kwenda katika muji wake mwenyewe. Kule akaanza kuwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, nao walishangaa na kuuliza: “Huyu amepata hekima na miujiza hii kutoka wapi?


Paulo alipokuwa akijitetea vile, Festo akamwambia kwa sauti kubwa: “Wewe Paulo, uko na wazimu! Elimu yako nyingi imekuvuruga kichwa.”


Walinzi wakajibu: “Hatujasikia mutu akisema sawasawa na mutu yule!”


Na wote waliomusikia walishangaa kuona akili yake na majibu yake.


Nao waliposikia jibu hili, wakashangaa sana, wakamwacha Yesu na kujiendea.


Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani.


Makundi ya watu waliposikia maneno hayo, wakashangaa sana na mafundisho yake.


Watu waliomufahamu Saulo zamani, walipomwona anatabiri, wakaulizana: “Kitu gani kimemupata mwana wa Kisi? Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”


Wayuda walikuwa wakimutafuta kwenye sikukuu ile na kuuliza kwamba yeye yuko wapi.


Lakini hakuna mutu aliyesema juu yake waziwazi, kwa sababu waliwaogopa wakubwa wa Wayuda.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Na ukimupa mutu yeyote asiyejua kusoma, na kumwambia “Unisomee kitabu hiki”, atasema: “Sijui kusoma.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite