Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Lakini hakuna mutu aliyesema juu yake waziwazi, kwa sababu waliwaogopa wakubwa wa Wayuda.

Gade chapit la Kopi




Yoane 7:13
13 Referans Kwoze  

Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliogopa wakubwa wa Wayuda. Wakubwa wale walikuwa wamekwisha kupatana kwamba mutu yeyote anayesadiki kuwa Yesu ndiye Kristo, atatengwa asiingie katika nyumba ya kuabudia.


Nyuma ya mambo hayo, Yosefu, mutu wa Arimatea, akamwomba Pilato ruhusa ya kuondoa maiti ya Yesu. (Yosefu alikuwa mumoja wa wanafunzi wa Yesu lakini kwa siri, kwa sababu aliwaogopa wakubwa wa Wayuda.) Pilato akamuruhusu. Basi Yosefu akaenda na kuondoa maiti ya Yesu.


Magaribi ya ile ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi walikusanyika katika nyumba na milango ilikuwa imefungwa, kwa sababu waliwaogopa wakubwa wa Wayuda. Mara moja Yesu akawatokea na kusimama katikati yao, akawaambia: “Amani kwenu!”


Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Kisha mambo hayo, Yesu akatembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea katika Yudea, kwa sababu Wayuda walitaka kumwua.


Wayuda walikuwa wakimutafuta kwenye sikukuu ile na kuuliza kwamba yeye yuko wapi.


Wayuda wakashangaa, wakisema: “Mutu huyu amepata elimu kama hii namna gani, naye hakufundishwa?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite