Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 6:60 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

60 Wengi kati ya wanafunzi wake waliposikia maneno haya, wakasema: “Masemi haya ni magumu. Ni nani anayeweza kuyakubali?”

Gade chapit la Kopi




Yoane 6:60
12 Referans Kwoze  

Basi kwa sababu ya maneno haya, wengi kati ya wanafunzi wake wakamwacha, nao hawakutembea tena pamoja naye.


Kwa sababu gani hamuelewi maneno ninayowaambia? Ni kwa sababu hamutaki kusikia maneno yangu.


Basi Yesu akawaambia wale Wayuda waliomwamini: “Kama mukitii mafundisho yangu, ninyi ni wanafunzi wangu hakika.


Heri mutu yule mimi sitakayekuwa kikwazo kwake!”


Ni vile ndivyo alivyoandika katika barua zote alimosema ndani yao juu ya mambo yale. Lakini ndani ya barua zile kunakuwa mambo mengine magumu kuyasikia. Na watu wajinga na wasiokamilika wanageuzageuza maana yake sawa vile wanavyogeuza sehemu zingine za Maandiko Matakatifu. Kwa njia ile wanajiangamiza wenyewe.


Tuna maneno mengi ya kusema juu ya jambo hili, lakini ni vigumu kuyaeleza kwenu kwa sababu ninyi mumekuwa na masikio magumu.


Yesu alialikwa vilevile kwenye ndoa ile pamoja na wanafunzi wake.


Kweli, kweli ninawaambia: kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wafu watakaposikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale wanaoisikia, wataishi.


Basi Wayuda wakaanza kubishana sana kati yao, wakasema: “Namna gani mutu huyu anaweza kutupatia mwili wake tuukule?”


Lakini kuna wengine kati yenu wasioamini.” (Yesu alisema vile kwa sababu alijua tangu mwanzo wale wasioamini na yule atakayemutoa.)


wandugu za Yesu wakamwambia: “Ondoka hapa, uende Yudea kusudi wanafunzi wako waone matendo unayofanya.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite