Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 6:53 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

53 Kwa hiyo Yesu akawaambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: musipokula mwili wa Mwana wa Mutu na kunywa damu yake, hamutakuwa na uzima ndani yenu.

Gade chapit la Kopi




Yoane 6:53
19 Referans Kwoze  

Yule anayekuwa na Mwana wa Mungu yuko na uzima ule, lakini yule asiyekuwa na Mwana wa Mungu hana uzima.


Mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.


Mukae ndani yangu, nami nitakaa ndani yenu. Tawi haliwezi kuzaa matunda lisipokaa ndani ya muzabibu. Vilevile ninyi hamuwezi kuzaa matunda musipokaa ndani yangu.


Kweli, kweli ninawaambia: anayeamini anapata uzima wa milele.


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”


na kusema: “Kweli ninawaambia: kama musipogeuka na kuwa sawasawa na mutoto mudogo, hamutaingia katika Ufalme wa mbinguni hata kidogo.


Yesu akajibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.


Hakika si vile: lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.”


Hakika si vile, lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.


Petro akamwambia: “Hautanawisha miguu yangu hata kidogo!” Yesu akamujibu: “Nisipokunawisha miguu, hauna ushirika pamoja nami.”


Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!


Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”


Basi itakuwa namna gani kama mukimwona Mwana wa Mutu akipanda tena pahali alipokuwa mbele?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite