Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 6:43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

43 Yesu akawajibu: “Musikuwe na manunguniko kati yenu.

Gade chapit la Kopi




Yoane 6:43
7 Referans Kwoze  

Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


Lakini kuna wengine kati yenu wasioamini.” (Yesu alisema vile kwa sababu alijua tangu mwanzo wale wasioamini na yule atakayemutoa.)


Yesu alitambua kwamba walitaka kumwuliza. Basi akawaambia: “Munaulizana juu ya maneno niliyosema kwamba kunabaki wakati kidogo nanyi hamutaniona, lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena?


Walipofika Kapernaumu na kuingia ndani ya nyumba, Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Mulibishana juu ya nini katika njia?”


Yesu akatambua maneno waliyosema, basi akawauliza: “Ee ninyi wenye imani ndogo, sababu gani munasemezana kati yenu juu ya kukosa mikate?


Nao wakasema: “Huyu si Yesu mwana wa Yosefu? Si tunawajua baba yake na mama yake? Namna gani anaweza kusema sasa kwamba alishuka toka mbinguni?”


Hakuna mutu anayeweza kuja kwangu, isipokuwa anavutwa na Baba aliyenituma, nami nitamufufua siku ya mwisho.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite