36 Lakini kama nilivyowaambia: mumeniona, lakini ijapokuwa vile hamuamini.
Ingawa vitambulisho vyote alivyoonyesha mbele yao, hawakumwamini,
Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: hamunitafuti kwa sababu muliona vitambulisho nilivyoonyesha, lakini kwa sababu mulikula mikate na kushiba.
Lakini Abrahamu akamwambia: ‘Kama wandugu zako hawasikilizi maonyo ya Musa na ya manabii, hawatasadiki hata mutu aliyefufuka.’ ”
Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.
Lakini kuna wengine kati yenu wasioamini.” (Yesu alisema vile kwa sababu alijua tangu mwanzo wale wasioamini na yule atakayemutoa.)
Hakika mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mutu anayemwona Mwana na kumwamini apate uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.”
Wakamwuliza: “Basi utatuonyesha kitambulisho gani kusudi tupate kukiona na kukuamini? Utafanya jambo gani?
Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.