Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 6:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: Musa hakuwapa ninyi mukate wa mbinguni, lakini ni Baba yangu anayewapa ninyi mukate wa kweli wa mbinguni.

Gade chapit la Kopi




Yoane 6:32
14 Referans Kwoze  

“Mimi ni muzabibu wa kweli, na Baba yangu ni mulimaji.


Huu ndio mukate ulioshuka toka mbinguni, nao si kama mukate ule babu zenu waliokula katika jangwa na kufa. Anayekula mukate huu ataishi milele.”


Halafu Yawe akamwambia Musa: “Mimi nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Kila siku watu watatoka na kukusanya chakula cha siku hiyo. Kwa njia hii nitawapima nione kama watafuata sheria zangu au hawatazifuata.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.


Lakini ule ni mukate ulioshuka toka mbinguni, anayeukula hatakufa.


Basi Wayuda wakaanza kunungunika kwa sababu Yesu alisema kwamba yeye ni mukate ulioshuka toka mbinguni.


Yesu akawaambia: “Mimi ni mukate wa uzima. Anayenikubali hatasikia njaa hata kidogo, na yule anayeniamini hatasikia kiu hata kidogo.


Maana mukate Mungu anaoupana ni yule anayeshuka toka mbinguni na kuleta uzima katika dunia.”


Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia.


Hata hivyo aliamuru mawingu, akafungua milango ya mbingu;


Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Babu zetu walikula mana katika jangwa, kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Aliwakulisha kwa mukate uliotoka mbinguni.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite