Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 6:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: hamunitafuti kwa sababu muliona vitambulisho nilivyoonyesha, lakini kwa sababu mulikula mikate na kushiba.

Gade chapit la Kopi




Yoane 6:26
20 Referans Kwoze  

Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Watu wengine wote wanatafuta faida yao wenyewe, lakini hawashuguliki na Yesu Kristo.


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


na magomvi yasiyokuwa na mwisho ya watu wenye akili iliyokwisha kupotoka hata wamesahau ukweli kabisa. Ndio wale wanaozani kwamba dini ni njia ya kupata utajiri.


Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.


Kundi kubwa la watu wakamufuata, kwa sababu watu hao waliona vitambulisho alivyoonyesha kwa kuponyesha wagonjwa.


Hawakuambatana naye kwa moyo, hawakukuwa waaminifu kwa agano lake.


Wakati walipoona kama Yesu hakukuwa pale wala wanafunzi wake, wakajiingilia ndani ya vyombo vile na kwenda Kapernaumu kumutafuta Yesu.


Yesu akajibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


Lakini kuna wengine kati yenu wasioamini.” (Yesu alisema vile kwa sababu alijua tangu mwanzo wale wasioamini na yule atakayemutoa.)


Kwa hiyo Yesu akawaambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: musipokula mwili wa Mwana wa Mutu na kunywa damu yake, hamutakuwa na uzima ndani yenu.


Kweli, kweli ninawaambia: anayeamini anapata uzima wa milele.


Wakamwuliza: “Basi utatuonyesha kitambulisho gani kusudi tupate kukiona na kukuamini? Utafanya jambo gani?


Wakati Yesu alipotambua kama walitaka kuja kumutwaa kwa nguvu na kumuweka kuwa mufalme, akaondoka na kwenda tena kwa kilima peke yake.


Watu walipoona kile kitambulisho Yesu alichoonyesha, wakasema: “Hakika mutu huyu ndiye yule nabii aliyepaswa kuja katika dunia!”


Lakini kama nilivyowaambia: mumeniona, lakini ijapokuwa vile hamuamini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite