Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 5:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Munachunguza Maandiko Matakatifu, kwa maana munazani kuwa ndani yao mutapata uzima wa milele. Maandiko hayo ndiyo yanayonishuhudia,

Gade chapit la Kopi




Yoane 5:39
51 Referans Kwoze  

Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.


Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno niliyowaambia wakati nilipokuwa ningali pamoja nanyi, kwamba sherti yatimizwe maneno yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa, katika maandiko ya manabii na katika Zaburi.”


Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.


Yesu akawajibu: “Munadanganyika, kwa sababu ya kutojua Maandiko Matakatifu wala uwezo wa Mungu.


Musome katika kitabu cha Yawe: Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana, kila kimoja kitakuwa na mwenzake. Maana kinywa cha Yawe kimeamuru hivyo. Roho yake itawakusanya hao wote.


Wakaaji wa Yerusalema na wakubwa wao hawakumutambua Yesu wala maandiko ya manabii yaliyosomwa kila siku ya Sabato. Lakini ingawa hivi wakatimiza maandiko yale kwa njia ya kumuhukumu kufa.


Kama mungemusadiki Musa, mungenisadiki mimi vilevile, kwa sababu yeye aliandika habari juu yangu.


Wenye hekima kati yenu wanafezeheka, watahangaishwa na kunaswa. Wamelikataa neno la Yawe. Basi ni hekima gani wanayokuwa nayo?


Kuna faida kubwa sana kila upande. Kwanza, Mungu alifunua Neno lake kwa Wayuda kusudi walishike.


Hamujasoma bado Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.


Nikaanguka mbele yake kusudi nimwabudu, lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe na wandugu zako wanaoshika ukweli ulioshuhudiwa na Yesu. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu! Maana ukweli ambao Yesu alishuhudia, ndio uwezo unaowaongoza manabii.”


Habari Njema hiyo iliahidiwa na Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake katika Maandiko Matakatifu.


Ee Mufalme Agripa, unaamini maneno manabii waliyosema? Ninajua kama unayaamini!”


Wakamujibu: “Na wewe vilevile umetoka Galilaya? Uchunguze Maandiko Matakatifu, nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki nabii.” [


Lakini kuna mwingine anayenishuhudia, nami ninajua kwamba ushuhuda anaoutoa juu yangu ni wa kweli.


Unawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako; unawakunywesha katika muto wa wema wako.


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


Lakini mimi nina ushuhuda mukubwa zaidi kuliko ule uliotolewa na Yoane. Maana sasa mambo ninayofanya ndiyo Baba aliyoniamuru kutimiza, nayo yananishuhudia na kuonyesha kwamba yeye amenituma.


Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Unanionyesha njia ya kufikia uzima. Kuwa mbele yako ni kujazwa furaha, kuwa kwa kuume kwako kunapendeza milele.


Lakini Abrahamu akamwambia: ‘Kama wandugu zako hawasikilizi maonyo ya Musa na ya manabii, hawatasadiki hata mutu aliyefufuka.’ ”


Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.


Hakikisha kwamba hautakisahau hata kidogo kitabu hiki cha sheria; lakini kila siku utajifunza kitabu hiki, muchana na usiku, kusudi upate kutimiza yote yaliyoandikwa humu, nawe utastawi na kufanikiwa.


Maana sheria hii si maneno matupu lakini ni uzima wenu; kwa njia ya sheria hii, mutaishi maisha marefu katika inchi munayokwenda kurizi, ngambo ya muto Yordani.”


Lakini kwa hakika walitamani sana inchi inayokuwa bora zaidi, ndiyo inchi ya mbinguni. Kwa sababu hii Mungu hasikii haya kuitwa Mungu wao, maana amewatayarishia muji.


Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.


Abrahamu akajibu: ‘Wandugu zako wako na maandiko ya Musa na ya manabii, wayasikilize!’


Wengi wa wale ambao wamekwisha kufa, watafufuka; wengine watapata uzima wa milele, na wengine watapata haya na kuzarauliwa milele.


Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”


Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Umemufikia, ukamupatia baraka nzurinzuri; umemuvalisha taji ya zahabu safi juu ya kichwa chake.


lakini anafurahia sheria ya Yawe, na kuifikiri muchana na usiku.


Ni kama umande wa mulima Hermoni, unaoanguka juu ya vilima vya Sayuni! Kutoka huko Yawe anatoa baraka, ndio uzima wa milele.


Kwa njia ya imani, wanawake wamoja walifufuliwa na kurudishiwa wale waliofiwa nao. Wengine waliteswa mpaka kufa, nao wakikataa kuachiliwa kusudi wapate ufufuko unaokuwa bora zaidi.


Basi Yesu akawaambia: “Enyi wajinga na wenye mioyo mizito kwa kuamini maneno yote manabii waliyosema!


lakini ninyi hamutaki kuja kwangu mupate uzima.


Yesu akajibu: “Musa aliwaamuru nini?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite