Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 5:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Kwa maana Baba anamupenda Mwana, anamwonyesha yote anayofanya yeye mwenyewe. Atamwonyesha mambo makubwa zaidi kuliko haya kusudi mupate kushangaa.

Gade chapit la Kopi




Yoane 5:20
17 Referans Kwoze  

Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Maana alipokea heshima na utukufu toka kwa Mungu Baba, wakati sauti yenye utukufu mukubwa toka kwa Mungu ilipomufikia ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana!”


Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”


Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.


Kweli, kweli ninawaambia: yeye anayeniamini atafanya vilevile matendo ninayofanya. Na zaidi ya ile atafanya matendo makubwa kuliko haya, kwa sababu ninakwenda kwa Baba.


Yesu akawaambia tena: “Nimewaonyesha matendo mengi mazuri kwa uwezo wa Baba. Ni kwa sababu ya tendo gani kati ya hayo munataka kunitupia mawe?”


na kutoka ndani ya makaburi yao. Waliotenda mema watafufuka na kupata uzima, lakini waliotenda mabaya watafufuka na kuhukumiwa.


Kweli, kweli ninawaambia: kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wafu watakaposikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale wanaoisikia, wataishi.


Kwa maana kama vile Baba anavyofufua wafu na kuwarudishia uzima, vile vile Mwana anawapa uzima wale anaowataka.


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Shetani akamupeleka tena mpaka juu ya mulima murefu, akamwonyesha falme zote za dunia na utajiri wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite