12 Basi wakamwuliza kwamba ni nani aliyemwambia kwamba atwae kipoyi wake na aende.
Yesu akaingia ndani ya hekalu. Alipokuwa akifundisha, wakubwa wa makuhani pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka yale?”
Kwa maana ninashuhudia kwamba wanajitoa kwa bidii kutumikia Mungu, lakini bidii ile haitokani na ufahamu wa kweli.
Wakaulizana: “Ni nani amefanya jambo hili?” Walipofanya uchunguzi wakagundua kwamba ni Gideoni mwana wa Yoasi ndiye aliyekuwa amefanya hayo.
Saulo akasema: “Mukuje hapa enyi viongozi wa watu, tujue ni zambi gani tumetenda leo.
Akawajibu: “Yule aliyeniponyesha ndiye aliyeniambia: ‘Twaa kipoyi chako na uende.’ ”
Lakini mutu yule aliyeponyeshwa hakujua ni nani, kwa maana Yesu alikuwa amekwisha kuondoka katikati ya kundi kubwa la watu waliokuwa pale.