Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 4:48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

48 Basi Yesu akamwambia: “Ninyi hamuwezi kuamini hata kidogo kama musipoona vitambulisho na maajabu.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 4:48
29 Referans Kwoze  

Na Yesu akamwambia: “Umeamini kwa sababu umeniona? Heri wale wanaoamini pasipo kuona!”


Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.


Wayuda wanaomba kuonyeshwa vitambulisho nao Wagriki wanatafuta hekima.


Lakini nikaota ndoto iliyonitisha; nikiwa nimelala katika kitanda, mawazo na maono yaliniogopesha.


“Ninyi wanainchi wenzangu Waisraeli, musikilize maneno haya: Yesu wa Nazareti alikuwa mutu aliyetambulishwa wazi na Mungu mbele yenu kwa njia ya vitambulisho, miujiza, na maajabu aliyofanya katikati yenu kama munavyojua ninyi wenyewe.


Ingawa vitambulisho vyote alivyoonyesha mbele yao, hawakumwamini,


Matendo yanayohakikisha kwamba mimi ni mutume yamefanyika kati yenu kwa uvumilivu wote, kwa njia ya miujiza, maajabu, na vitambulisho.


kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.


Paulo na Barnaba wakakaa Ikonio kwa muda murefu. Walisema kwa uhodari kabisa, wakimutumainia Bwana. Naye aliwapa uwezo wa kufanya maajabu na vitambulisho. Na kwa njia hiyo alihakikisha kwamba ujumbe walioutangaza juu ya neema yake ulikuwa wa kweli.


Kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao watafanya vitambulisho na maajabu, kusudi ikiwezekana wawadanganye wachaguliwa wa Mungu.


kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.


Kila mumoja wao akaingiwa na woga, nao mitume walifanya maajabu na vitambulisho vingi.


Basi Wayuda wakamwuliza: “Utaonyesha kitambulisho gani kwa kutuhakikishia kwamba uko na haki ya kufanya hivi?”


Lakini Abrahamu akamwambia: ‘Kama wandugu zako hawasikilizi maonyo ya Musa na ya manabii, hawatasadiki hata mutu aliyefufuka.’ ”


Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?


Mwovu atakuja na uwezo wa Shetani na kufanya miujiza ya kila namna, vitambulisho na maajabu ya uongo.


Basi mukutano wote ukabaki kimya ukisikiliza maelezo ya Barnaba na Paulo juu ya vitambulisho na maajabu yote Mungu aliyofanya kwa njia yao katikati ya watu wa mataifa mengine.


Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


Stefano alijaliwa sana na neema ya Mungu na alikuwa na uwezo mwingi, naye alifanya maajabu na vitambulisho vikubwa katikati ya watu.


Mitume walifanya maajabu na vitambulisho vingi katikati ya watu. Waamini wote walizoea kukusanyika katika Baraza wanaloliita La Solomono.


Utumie nguvu zako kwa kuponyesha watu, kwa kufanya maajabu na vitambulisho kwa uwezo wa jina la mutumishi wako mutakatifu Yesu.”


Nami nitafanya maajabu juu katika mbingu na vitambulisho chini katika dunia: kutakuwa damu, moto na moshi mwingi.


Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.


Naye Yesu akamwambia: “Nilimwona Shetani akianguka kama umeme toka mbinguni.


“Aliokoa wengine, lakini sasa anashindwa kwa kujiokoa yeye mwenyewe! Yeye ni mufalme wa Waisraeli, sasa ajishushe pale juu ya musalaba kusudi nasi tupate kumwamini.


Wafarisayo na Wasadukayo wakamufikia Yesu. Nao wakamupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake unatoka kwa Mungu.


Ninatoa amri katika ufalme wangu kwamba watu wote wanapaswa kumwogopa na kumuheshimu Mungu wa Danieli. Yeye ni Mungu Mwenye Uzima, anayeishi milele; ufalme wake hauwezi kuangamizwa hata kidogo, utawala wake hauna mwisho.


Yule mukubwa wa serikali akamujibu: “Bwana, ninakuomba ufike kwangu mbele mutoto wangu hajakufa.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite