Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 4:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Na Wasamaria walipomufikia Yesu, walimusihi akae pamoja nao, naye akakaa kule muda wa siku mbili.

Gade chapit la Kopi




Yoane 4:40
15 Referans Kwoze  

Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Lakini wakamusihi sana abakie pamoja nao, kwa maana ilikuwa magaribi na giza lilitaka kuingia. Basi akaingia ndani ya nyumba kubakia pamoja nao.


Mutu yule aliyeponyeshwa pepo akamusihi Yesu aende pamoja naye, lakini akamukatalia, akimwambia:


Wewe unayekuwa tumaini la Waisraeli, wewe unayetuokoa wakati wa taabu, namna gani unajifanya kama mugeni katika inchi, kama musafiri anayelala kwa usiku mumoja tu?


Mara tu nilipoachana nao, nikamwona mupenzi wangu wa moyo. Nikamushika wala sikumwacha aondoke, mpaka nilipomupeleka katika nyumba kwa mama yangu, mpaka ndani ya chumba cha yule aliyenizaa.


Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.


Mutu yule alipoona kwamba hawezi kumushinda Yakobo, alimugusa Yakobo kwenye maunganio ya kiuno, naye akateguka alipokuwa anapigana naye.


Marta alikuwa na dada yake mudogo aliyeitwa Maria. Huyo aliikaa mbele ya Bwana, akisikiliza mafundisho yake.


Wasamaria wengi wa muji ule walimwamini Yesu kwa sababu ya maneno ya yule mwanamuke aliposhuhudia hivi: “Aliniambia mambo yote niliyotenda.”


Wengine wengi zaidi waliamini kwa sababu ya maneno yake mwenyewe,


Siku mbili zilipopita, Yesu akaondoka kule, akaenda Galilaya.


Hivi kukakuwa furaha kubwa katika muji ule.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite